Snoop Dogg Alipoteza Fahamu Baada ya Kumuona 2 Pack Akiwa Mahututi Hospitalini - EDUSPORTSTZ

Latest

Snoop Dogg Alipoteza Fahamu Baada ya Kumuona 2 Pack Akiwa Mahututi Hospitalini


Snoop Dogg amefunguka kwamba alipoteza fahamu baada ya kumuona Tupac Shakur akiwa mahututi hospitali mara baada ya kupigwa risasi September 7, 1996.

Akizungumza kwenye podcast ya Logan Paul ‘Impaulsive’ Snoop Dogg amesema kabla ya kufika alihisi mambo yataenda kuwa sawa lakini baada ya kumuona mshkaji wake anapumulia mpira ndipo alihisi hali sio shwari.

Mama mzazi wa Tupac Shakur alimchukua na kumpeleka bafuni kwa ajili ya kuzungumza naye namna ya kuwa imara juu ya jambo lile. Baadaye Snoop alirejea kwenye nguvu na kwenda kuzungumza na Tupac ambaye walikuwa marafiki wakubwa. Na hiyo ilikuwa ndio mara ya mwisho kuzungumza naye, September 13 alitangazwa kufariki.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz