OMMY DIMPOZ AMLILIA DIAMOND - EDUSPORTSTZ

Latest

OMMY DIMPOZ AMLILIA DIAMOND



Diamond na Ommy Dimpoz waliwahi kuwa marafiki wa kutupwa kabla upepo haujabadilika
Pichani:Wasanii Ommy Dimpoz na Diamond Platnumz
Jamii nzima ya wapenda burudani Tanzania na Afrika kwa ujumla WA nafahamu fika kwamba Jana,tarehe 13 ya Septemba ilikuwa siku maalumu mwa mwanamuziki KIPENZI cha watu Tanzania na Afrika Mashariki pamoja na watu wengine wote waliozaliwa siku kama hiyo Ulimwenguni.
Yawezekana kwa OMMY Dimpoz ILIKUWA ni siku ya FURAHA zaidi hasa kufuatia matatizo amabayo ameyapitia KIPINDI cha nyuma ambao aliugua kiasi kufika hatua ya kufanyiwa upasuaji wa koo Nchini Afrika Kusini,huku hali MBAYA ikimrudia wiki tatu zilizopita na kuamsha kazi ya ziada kwa watu mbalimbali kumuombea Uzima na AFYA.
Katika mahojiano aliyoyafanya na Millard Ayo,Ommy alieleza chanzo cha maradhi yake kuwa aliwekewa sumu kwenye chakula na mtu ambaye ALIKUWA na lengo la kumtoa roho.
Hayo wakati yanamkuta na kumfanya apitie mtihani mgumu kstika maisha yake watu wote wa sanaa waliwekeza nguvu zao huko kwa maombi na kumjulia hali Mara kwa mara.Lakini kitu cha ajabu ni kwamba aliyewahi kuwa rafiki yake kipenzi Diamond pamoja na meneja wake Mubenga hawakuwahi kumjulia hali hata siku moja.Moja ya Maneno aliyoyaongea OMMY alisema "kuumwa kwangu imekuwa ni ibada kwangu pia"
Katika siku yake hiyo ya kumbukumbu ya kuzaliwa ommy dimpoz aliandika kirefu ujumbe ufuatao;
ommydimpozLeo 13th September ni kumbukumbu yangu ya siku ya kuzaliwa. 

Namshukuru sana Mwenyezi Mungu (ALHAMDULILAAH) kwa kunipa nafasi ya kuuona mwaka mwingine, kwani niliyoyapitia katika kipindi cha takribani miezi 5 kama ingekuwa sio mapenzi yake yeye (M/Mungu) basi ingekuwa imebaki history. 
Nilichojifunza kipindi hichi chote ni kuwa kuumwa ni Ibada na sisi kama binadamu hatujakamilika leo unaweza kuwa mzima na kesho ukawa mahututi kitandani, ndio maana nimeamua kushare picha ambayo nilipigwa nikiwa ICU japo nafahamu sio kitu kizuri kupost picha kama hii kwenye mitandao ila nia yangu ni kujaribu kukumbushana sisi kama Binadamu kuwa kuna leo na kesho kwahiyo tusiishi kwa chuki na Uadui maana hatujui kesho yetu itakuwaje!! Kuna kipindi wakati nimelazwa nilikata tamaa ya kuishi nikaona labda muda wangu umekwisha lakini hapo Hospital akaletwa mgonjwa mwingine ambae alikuwa pembeni yangu alishambuliwa na majambazi kwa risasi tisa mwilini lakini madaktari wakafanikiwa kuokoa maisha yake na akapona so nikajiuliza mimi ni nani nikate tamaa ya kuishi na nikajifunza kwamba kuugua sio kufa, Ni vyema tukipata nafasi basi tuwaombee na kuwafariji wagonjwa kwani wanayoyapitia ni magumu mno. Kwasasa namshukuru Mwenyezi Mungu naendelea vizuri na bado niko kwenye recovering,

pia nawashukuru watu wote ambao mmekuwa mkiniombea dua nipone kwa haraka kuanzia mashabiki mpaka wasanii wenzangu na kila mtu aliyeniombea kwa imani yake Nashukuru sana. Mungu awabariki sana.
:
Pia Shukran za dhati kwa Familia yangu, Marafiki zangu wa Karibu, Management yangu ROCKSTAR FAMILY @officialalikibana my lovely Manager @sevenmoshaambaye amehangaika na mimi mfano wa Mama Mzazi na mtoto wake pamoja na my Big Brother Governor @joho_001 ambaye ameniuguza kwa kipindi hichi chote chini ya uangalizi wake na Madaktari kuanzia Kenya Mpaka South Africa.
ASANTENI SANA NA INSHAALLAAH KWA UWEZO WA ALLAAH I WILL COME BACK STRONGER 💪🏽🙏❤






Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz