DIAMOND KUTIMIZA AHADI NA IRENE UWOYA - EDUSPORTSTZ

Latest

DIAMOND KUTIMIZA AHADI NA IRENE UWOYA


Pichani:Mwanamuziki Diamond Platnumz kushoto na mwanamitindo Irene Uwoya kulia
Kile kitendawili ambacho kimetegwa huenda punde kikapata jibu bila ya hata mtegaji kupewa mji ili atupatie jibu.Na kwa hakika hii italeta faraja kubwa sana na furaha kwa wapenda burudani na familia kwa ujumla kwani mpaka sasa imeonekana kuwa tatizo kwa Msanii huyo
Ukiachilia mbali skendo inayomuandama kwa sasa kuhusiana na uwepo wa fununu ya kwamba ameendewa kwa sangoma ili afungwe na kutulizwa mzuka na sangoma kunakodaiwa kutekelezwa na mlimbwende,video vixen na mwanamitindo Hamisa Mobetto,skendo ya kutoonyesha upendo wowote kwa OMMY DIMPOZ,Msanii Diamond Platnumz amedhamiria kufanya jambo hili.

September 6 kulizuka sintofahamu baada ya mwanamuziki staa kutoka kiwanda cha BURUDANI Tanzania na mkali wa kibao cha #jibebe Diamond Platnumz kupitia ukurasa wake wa Instagram kupost picha ya mwanadada mkali kunako kiwanda cha filamu na mitindo hapa bongo Irene UWOYA.
Sio kawaida kabisa kwa diamond kutumia ukurasa zake za mitandao ya kijamii kupost watu ambao hana malengo nao,na inaaminika ya kwamba ukiona hivo basi JUA kuna jambo.
Kupitia mitandao mbalimbali ikiwepo you tube kumekuwa na ripoti kwamba kuna uwezekano mkubwa ndoa ya Dogo Hanna na Irene Uwoya UKAWA inevunjika hasa baada ya Irene Uwoya kusafiri peke yake kuelekea Dubai ambao haijafahamika rasmi naenda kufanya nini na ndicho kipindi ambacho Diamond ambaye ni CEO wa WCB Company alipompost na kuzua mjadala.WENGI wanaamini ya kwamba Diamond anaweza kumuoa Irene Uwoya hasa kutoka na na kuonekana anajielewa sana tofauti na WANAWAKE wengine kadhaa ambao Diamond KATIKA nao kimapenzi ukimuondoa Zari.

Pichani:Hamisa Mobetto,Diamond Platnumz na Zarina Hassan

Lakini moja kati ya mambo ambayo yameanza kujitokeza ni kwamba tayari Irene kashapewa shavu kupitia WAsafi Tv kuhost project ya shindano ka Niko Jibebe ambao inefahamika kwamba atakuwa Jaji mkuu.
Pamoja na mwanamuziki mkali kutoka A-town anayetamba na kibao cha #banana Dogo Janja kuelezea kutokuwa na wasiwasi na mkewe na kwamba anamuamini huku akisisitiza kwamba kamwacha mkewe aende ughaibuni peke yake kwani hawawezi fuatana KILA mahali lakini bado kuna zusha maswali hata kuonekana ukaribu Wao INSTAGRAM ukiwa unepungua.

Watu wanaendelea kusubiri Kuona ahadi ya Diamond aliyoitoa MWEZI February,2018 kwa Mama yake na mashabiki wake kwamba lazima AKE mwaka huu kufuatia kuachana na Zari KATIKA hali ya kutatanisha,bado ni kitendawili,nani atamuoa kati ya WANAWAKE watatu wa mwanzo Wema  Sepetu,Hamisa Mobetto aliyezaa nae mtoto MMOJA na Zari AMBAYE NAPATA naye Watoto wawili huku akiongezeka Irene Uwoya.

TAFADHALI NINI MAONI YAKO,NANI ANAMFAA DIAMOND KATI YA WANAWAKE WANNE HAPO JUU?.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz