MANENO YA ZITO KABWE BAADA POLEPOLE KUMKOSOA KUHUSU UPOTEVU WA 1.5T - EDUSPORTSTZ

Latest

MANENO YA ZITO KABWE BAADA POLEPOLE KUMKOSOA KUHUSU UPOTEVU WA 1.5T


Mhe Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa ACT Maendeleo
Zitto kabwe Mbuge wa Jimbo la kigoma mji na Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo kupitia ukurasa wake wa twitter na facebook amejibu hoja za katibu wa itikadi na uenezi wa CCM humphrey polepole aliyesema zitto kabwe anapotosha UMMA juu ya tuhuma za upotevu wa trion 1.5 kulingana na repoti ya CAG Kama anvyo dai Mh Zitto Kabwe.

Polepole pia amesema kuwa Zitto kabwe ana bahati kwa kua rais JPM ni mpole vinginevyo angekua ameisha chukuliwa hatua kwani alizoeshwa vibaya. Pia amesisitiza kuwa anapaswa kuchukuliwa hatua kwani anapotesha repoti ya CAG


Zitto Kabwe ame yaandika haya
Kuna mtu anasema nikamatwe kwa kupotosha Kuhusu TZS 1.5trn zinazohojiwa na CAG.
Mimi Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto, Mwenyeji wa Kigoma, Muislam, NAAPA kwamba Serikali ya CCM ya Awamu ya Tano imeshindwa kuonyesha kwa CAG matumizi ya shilingi trilioni MOJA na Bilioni MIA TANO.
Nipo tayari kukamatwa kwa kusema hivyo ( haitafuta ukweli wa ubadhirifu huo ). Nipo tayari kuuwawa kwa kusema hivyo ( mawazo yangu hayatakufa).
Eeh Mwenyezi Mungu nisaidie.
Pia Zitto ameendelea kusisitiza kuwa anao uzoefu wa kutosha wa miaka 8 akitumikia PAC na POAC hivyo nidhahiri ya kuwa trioni 1.5 ya watanzania haina maelezo ya matumizi yake. 
EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati.
Enter your email address:


Delivered by EDUSPORTSTZ
Subscribe to EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz