POLEPOLE ALIAMSHA DUDE-AITETEA REPORT YA CAG KWA KUMVAA ZITTO PAMOJA NA UPINZANI - EDUSPORTSTZ

Latest

POLEPOLE ALIAMSHA DUDE-AITETEA REPORT YA CAG KWA KUMVAA ZITTO PAMOJA NA UPINZANI




Katibu wa Itikadi na uenezi CCM, Humphrey Polepole anaongea na waandishi wa habari kuhusu ripoti ya CAG

Polepoele anasema kuna viongozi wa vyama vya siasa wanapotosha ripoti hiyo na inafaa iwekwe utaratibu waanze kuchukuliwa hatua

Polepole amesema kuna kiongozi mmoja wa upinzani amekuwa akizungumza uwongo na kuleta taharuki kwa wananchi na kusema inafaa achukuliwe hatua ili aach

Polepole amesema anaipongeza serikali ya CCM kwa kuweka utaratibu mzuri wa kuweka hadharani ripoti ya CAG na kuchukua hatua kwa wanaofanya ubadhirifu unaobainishwa.

Polepole anaipongeza serikali kwa kuwa Rias Magufuli alipochukua hatua za awali, mawaziri nao walifuta hatua hizo na kuwachukulia hatua maafisa kwenye wizara zao

Polepole amesema pia vipo vyama vya siasa vinatumia fedha ya umma na havitoi hesabu na kusemainabidi vichukuliwe hatua kali za kinidhamu


Amesema vipo vyama vimetumia zaidi ya Sh. milioni 700 bila kutoa hesabu, pia vipo vyma ambavyo vinatumia fedha bila kufuata kanuni za kihasibu

Kuna chama kinaitwa ABC, SAU, CHADEMA wametumia fedha bila kutoa hesabu zilivyotumika na pia kutumia fedha zaidi ya bilioni 2.2 bila kupeleka benki na kuhoji vinawezaje kuikosoa serikali?

Pia CHADEMA imefanya manunuzi ya zaidi ya bilioni 24 bila kushindanisha wakati ndio hao wanaoisema serikali


Polepole anasema isiidhie kuwataja kwenye taarifa ila msajili achukue hatua, hata kama ni ndani ya CCM


Polepole amesema inapotoshwa kuwa CCM imekopa ndani ya mifuko ya hifadhi ya jamii, CCM ina utaratibu wake wa ndani wa kulinda maslahi ya watumishi wake tofauti na vyama vingine


CCM ina utaratibu wa kulimbikiza fedha kila mwisho wa mwezi ili watumishi wake wanapomaliza utumishi, ipo fedha ya kuwalipa mafao yao

Katika akaunti ya CCM inayosimamiwa na Baraza la wadhamini walitoa zaidi ya milioni 300 ili watumishi wanaaondoka walipwe na wanazirudisha ili mfuko uendelee kunona

Amesema CHADEMA wamepotosha juu ya hili na wanapaswa kuchukuliwa hatua

Polepole pia anasema serikali ya CCM sasa ina utaratibu wa kuweka hesabu za serikali katika mtindo jumuishi, zamani zilikuwa zikitolewa kwa wizara na taasisi moja moja lakini kwa sasa unaweza kuzipata katika sehemu moja

Tanzania ni nchi ya pekee kufanya hivyo katika Afrika Mashariki na hii inasaidia kuweka mambo wazi zaidi na mtindo huu ni mgumu

Polepole amesema Zitto Kabwe ndio anaongoza kupotosha ripoti ya CAG kwa kukurupuka naripoti asizozielewa, na kusema Taarifa ya CAG ilikuwa imeshapitiwa na wao kwanza

Polepole anasema anapotosha kuwa trilioni 1.5 zimepotea na kufafanua kuwa sasa kuna mtindo mpya ambao unafuata vigezo vya kimataifa vya ukaguzi wa hesabu za umma unaitaka serikali inapokagua fedha zake zinapoingia kuhesabu pia na pesa baada ya serikali kuwa imetoa huduma ,
zamani ilikuwa ni lzaima ipokee fedha kwanza ndipo ihesabu fedha imeingia, ila sasa huduma inapotolewa hata kama fedha haijakusanywa inahesabiwa (acrrual basis)

Makusanyo ghafi ni makusanyo ya jumla, baada ya makusanyo ghafi inatakiwa ukokotoe ujue makusanyo sahihi ni yapi

Tumekusanya trilioni 25.3, pesa ambayo huduma imetolewa na inatarajiwa imekushwa kuingizwa kwenye jumla hiyo

ukitaka kujua makusanyo halisi unachukua trilioni 25.3 unatoa makusanyo tarajiwa (receivables)


Unachukua trilioni 25.3 unatoa bilioni 687.3 (receivables) kama hatua kupata makusanyo halisi

Pia unatoa bilioni 203.92 ambazo ni fedha zilizokusanywa kwa ajili ya Zanzibar, ambayo haisomwi kwenye bajeti ya Serikali ya Muungano

Ukitoa hesabu hizo unapata Shilingi trilioni 24.4 hizi ndio makusanyo halisi ya mwaka 2017/208

Zitto anadai pesa zilizotumiaka kutoka trilioni 25.3 ni trilioni 23.79, hii kipindi mkaguzi anapita zilikuwepo fedha za serikali ambazo zilikuwa kwenye hatifungani (zilikuwa hazijaiva) ambayo ni shilingi 697.85 bilioni

Ukichukua 697.85 bilioni ukijumlisha trilioni 23.5 unapata trilioni 24.4, na ukichukua 25.3 ukatoa 23.79 unapata 1.5 trilioni ambayo ndio zitto anadai imeibiwa

Polepole anasema Zitto hajui hesabu na anapaswa kumtafuta mwalimu.

Polepole anasema pia Zitto amepotosha kuhusu bilioni 219 ambayo ililipa madeni ya zamni ambayo hayakuwa yamepitishwa na Bunge

Amesema haesabu za serikali zinawekwa kwenye vifungu, na kulikuwa na madeni ya watu mbalimbali yanayofikia bilioni 969 ambayo yalipitishwa na Bunge na serikali inayalipa baada ya kuyahakiki, bilioni 219 ni sehemu ya bilioni hizo 969 zinazofahamika na Bunge pia

Polepole amesema Zitto amepotosha pia kuhusu serikali kukopa bilioni 500 ambazo ni zaidi ya ukomo iliyowekewa, amsema hili hatajibu analiachia Bunge, hayo mawili ameyazungumzia ili kumpa elimu


Polepole amesema Zitto achukuliwe hatua kwa kupotosha na ni kwa sababu alikuwa amezoeshwa vibaya.

WEKA EMAIL YAKO HAPA KUTUMIWA HABARI


Delivered by EDUSPORTSTZ
Subscribe to EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz