Ahmed Ally Acharuka awapa mashabiki makavu yao ni kuhusu jambo hili

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amethibitisha kuwa mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Gaborone United ambao utapigwa Jumapili, Septemba 28 katika uwanja wa Benjamin Mkapa, hautahudhuriwa na mashabiki

Ahmed amesema Simba imeadhibiwa na CAF kutokana na matukio ya mashabiki kuvamia uwanja na kuwasha fataki ambazo zimepigwa marufuku msimu uliopta katika mchezo wa robo fainali kombe la Shirikisho (CAFCC) dhidi ya Al Masry

Ahmed amewaasa mashabiki wa Simba kuepuka matukio ya aina hiyo ili kukwepa adhabu nyingine katika mechi zijazo

Akizungumzia maandalizi ya mchezo huo, Ahmed amesema kikosi kilirejea kambini jana baada ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Fountain Gate ambao Simba iliibuka na ushindi wa mabao 3-0

"Tunafahamu ya kwamba tuna mechi ya Ligi ya Mabingwa siku ya Jumapili kwenye dimba la Mkapa kuanzia saa 10 jioni na tayari wageni wetu Gaborone United wamewasili alfajiri ya leo. Mambo yote yamekwenda vizuri na watafanya mazoezi leo na kesho."

"Mchezo wetu wa Jumapili utachezeshwa na waamuzi kutoka nchini Niger na sasa wapo njiani. Kikosi kiliingia kambini jana baada ya mchezo dhidi ya Fountain Gate walirudi kambini na wapo timamu, hakuna mtu yeyote ambaye alipata majeraha. Watakaokosa mchezo ni Mohammed Bajaber na Abdulrazak Hamza."

"Nipo hapa kuwathibitishia kwamba mechi yetu ya Jumapili haitakuwa na mashabiki kutumikia adhabu ya CAF. Kilichosababisha ni mchezo ni dhidi ya Al Masry, kuna shabiki aliingia uwanjani na kuna mashabiki waliwasha moto."

"Adhabu hiyo inakwenda pamoja na faini ya Dola 50,000 kama Tsh. 120 milioni hivi. Niwaase mashabiki wenzangu wa Simba, uache vitendo vya vurugu uwanjani. Kwanza tuanze ulinzi wa wenyewe kwa wenyewe ukiona mtu anataka kuwasha zile fire works mzuie, ukiona mtu anataka kuingia uwanjani tushirikiane kumzuia ikiwezekana kumtoa uwanjani. Angalia mechi kama hii tunakwenda uwanjani bila mashabiki. Hatupo hapa kulaumiana ila kukumbushana,” alisema Ahmed

Usikose kutazama mechi hizi zote za LIGI KUU TANZANIA BARA, MECHI ZA ULAYA, MASHINDANO YA CAF LIVE bure kupitia Simu yako download App yetu mapema itakayokuwezesha kuzitazama mechi hizi live bure pia ndani ya App yetu utaweza kutazama chanel za Azam tv na Dstv bure bonyeza  HAPA  au Bonyeza HApa   Au hapa pia kudownload app kumbuka app bado hatujaiweka playstore hivo utaidownload kama Apk ikileta neno harmful usiogope.

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post