Simba kucheza mechi yao dhidi ya Gaborone bila mashabiki


 Klabu ya Simba italazimika kucheza bila ya mashabiki mechi ya mkondo wa pili hatua ya awali michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Gaborone United

Baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa Francistown huko Botswana, Jumapili Septemba 28 Simba itakuwa mwenyeji katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa, saa 10 jioni

Simba ilikata rufaa kwa Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) juu ya adhabu ya kuzuiwa kuingiza mashabiki katika mchezo huo, hata hivyo rufaa hiyo imekataliwa

Wekundu hao wa Msimbazi waliadhibiwa kufuatia matukio yaliyojitokeza msimu uliopita katika mchezo wa robo fainali CAFCC dhidi ya Al Masry ambapo mashabiki walivamia uwanja baada ya Simba kuibuka na ushindi wa mikwaju ya penati 4-1 na kutinga nusu fainali

Simba inahitaji ushindi au matokeo yoyote ya sare katika mchezo huo siku ya Jumapili ili kufuzu raundi ya kwanza

Mchongo huu hapa usikose kutazama mechi hizi zote za LIGI KUU TANZANIA BARA, MECHI ZA ULAYA, MASHINDANO YA CAF LIVE bure kupitia Simu yako download App yetu mapema itakayokuwezesha kuzitazama mechi hizi live bure pia ndani ya App yetu utaweza kutazama chanel za Azam tv na Dstv bure bonyeza  HAPA  au Bonyeza HApa   Au hapa pia kudownload app kumbuka app bado hatujaiweka playstore hivo utaidownload kama Apk ikileta neno harmful usiogope.

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post