CHAN 2024: Stars kamili kuikabili Burkinafaso ( Tazama hapa )

CHAN 2024: Stars kamili kuikabili Burkinafaso ( Tazama hapa )

Download App ya Nijuze Tv kutazama mechi za ligi kuu Nbc bure, Epl, Laliga, Bundesliga, Seria A, Caf na nyinginezo pia app hii ina chanel za Azam tv na Dstv utaweza kuzitazama bure

Idownload kwa kubonyeza HAPA au HAPA sisi kwetu michezo ni Furaha

Usikose kuitazama mechi za michuano ya CHAN na LIGI KUU TANZANIA BARA, MECHI ZA ULAYA LIVE bure kupitia Simu yako download App yetu itakayokuwezesha kuzitazama mechi hizi live bure pia ndani ya App yetu utaweza kutazama chanel za Azam tv na Dstv bure bonyeza HAPA kudownload app
Mashindano ya Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) yanatarajiwa kuanza rasmi leo , Agosti 02, 2025, kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, ambapo Tanzania (Taifa Stars) itamenyana na Burkina Faso katika mchezo wa ufunguzi utakaoanza saa 2:00 usiku.

Tanzania inakuwa mwenyeji wa mashindano haya kwa mara ya kwanza katika historia, kwa kushirikiana na Kenya na Uganda kama waandaaji wenza wa michuano hiyo ya Afrika.

Mchezo wa leo unatarajiwa kuwa na ushindani mkali, huku makocha wa timu zote mbili wakiweka wazi dhamira zao kuelekea mchezo huo

Mkufunzi wa Stars Hemed Morocco amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi kuwaunga mkono akiwahakikishia kikosi chake kiko tayari kwa michuano hiyo

"Tupo Tayari, Tuna Kikosi imara. Tupo tayari kukutana na timu yoyote katika mashindano haya kutokana na aina ya kikosi nilichonacho. Tumefanya maandalizi ya kutosha na wachezaji wote wako fiti,” alisema Morocco katika mkutano na wanahabari

Kocha huyo ameongeza kuwa michezo ya kirafiki waliyocheza kabla ya mashindano imesaidia kupunguza presha kwa wachezaji, hasa chipukizi waliopo kwenye kikosi hicho.

“Wachezaji chipukizi wameonyesha kiwango kizuri na kushirikiana vyema na wazoefu. Tunaamini tunaweza kufanya vizuri na kuacha kombe nyumbani,” alisisitiza.

Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, mlinda lango Aishi Manula alisema wanakwenda kupambana kulinda heshima ya nchi nyumbani

"Tutapambana Kulinda Heshima ya Nyumbani.Tunajivunia kucheza kwenye ardhi ya nyumbani. Tutapambana kuhakikisha tunashinda michezo yetu ya mwanzo,” alisema Manula. 
Usikose kuitazama mechi za michuano ya CHAN na LIGI KUU TANZANIA BARA, MECHI ZA ULAYA LIVE bure kupitia Simu yako download App yetu itakayokuwezesha kuzitazama mechi hizi live bure pia ndani ya App yetu utaweza kutazama chanel za Azam tv na Dstv bure bonyeza HAPA kudownload app

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post