Sajili zilizo Kamilika Mpaka sasa Yanga


 Jana Yanga ilitambulisha usajili wa kwanza katika dirisha hili, kiungo mkabaji Moussa Balla Conte aliyetua kutoka klabu ya CS Sfaxien

Conte alitua nchini mapema jana na kusaini mkataba wa miaka mtatu ambao utamuweka Jangwani hadi Julai 2028

Awali Yanga ilipanga kuanza kutoa taarifa za usajili siku ya Jumapili, Julai 20 lakini sintofahamu iliyogubika usajili wa nyota huyo ilipelekea viongozi wa Yanga kuamu kumaliza utata mapemaa kwani kuna propaganda zilikuwa zikifanywa kudai nyota huyo amegoma kucheza Yanga licha ya mabingwa hao wa nchi kumalizana na klabu yake

Huo ni usajili wa kwanza kutambulishwa, taarifa za usajili zitafahamika zaidi wiki ijayo ikiwa ni wiki ya mwisho kabla ya taratibu za pre-season kuanza

Juzi wakati akizungumza na chombo kimoja cha habari, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe alidokeza kuwa mpaka sasa bado usajili wa mchezaji mmoja tu ili Yanga kufunga hesabu zake za usajili katika dirisha hili

Kwa mujibu wa taarifa za ndani, hawa hapa wachezaji ambao tayari wamemalizana na Yanga;

Mohamed Doumbia (CM)

Moussa Balla Conte (DM)

Abdulnasir Mohammed (DM)

 Aboubakar Nidhar Otham (CB)

Offen Chikola (AM)

Celestin Ecua (AM)

Kwa mujibu wa taarifa, hizi hapa sajiri zinazosubiri kukamilika;

Mohammed Hussein (LB)

Feisal Salum (AM)

Aidha inaelezwa kuwa Yanga inaweza kusajili nyota wengine wawili katika nafasi ya beki wa kati na mshambuliaji hasa endapo dili la Clement Mzize kuelekea Zamalek kama litakamilika

Yanga inahusishwa na walinzi wawili raia wa DR Congo, Hennock Inonga ambaye ni mchezaji huru baada ya kumalizana na FAR Rabat na Kevin Mondeko aliyesitisha mkataba wake na USM Alger

Huna sababu ya kukosa kutazama michuano ya CHAN LIVE kupitia Simu yako

Michuano hii itaanza Agosti 02, kwa mechi ya ufunguzi kuchezwa katika dimba la Benjamin Mkapa kwa wenyeji Taifa Stars kucheza dhidi ya Burkina Faso.

Usikose kuitazama michuano hii LIVE  bure kupitia simu yako  download App hii mapema inayorusha mechi zote live bure pia ukiwa na App yetu utaweza kutazama chanel zote za Azam Tv na DSTV live bure mfano Azam sport 1, Azam Two, Sinema zetu na nyingine nyingi pia App bado hatujaiweka playstore hivo italeta neno This file might be harmful usiogope


0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post