Yanga yakusanya Tsh Bil 17.8 - EDUSPORTSTZ

Latest

Yanga yakusanya Tsh Bil 17.8

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Katika Mkutano Mkuu wa Wanachama wa Yanga unaendelea ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam, klabu imetangaza mapato na matumizi kwa msimu uliopita huku wakitangaza bajeti kwa ajili ya msimu wa 2023/24


Katika msimu uliopita, Yanga ilikusanya jumla ya Tsh Bilioni 17.8 huku matumizi yakiwa Tsh Bilioni 17.3


Mchanganuo wake ni; Udhamini Bilioni 8.1, Mapato ya mlangoni Bil 2, Ada za uanachama Mil 939, Zawadi Bil 1.1, Mauzo ya wachezaji Mil 200, faida ya jezi Mil 337, Mengine Tsh Milioni 150, mikopo Bil 4.08


Baadhi ya matumizi ni pamoja na Mishahara Bil 5.4, ada za wachezaji Bil 2.4, motisha 2.8Bil, kambi Milioni 460, Chakula na Malazi Bil 1.1, maandalizi ya mechi Bil 1.4, usafiri Bil 1.6, kodi nyumba Mil 290, Matibabu Mil 102. Jumla matumizi Bil 17.3 na kubakiwa na Mil 581


Bajeti ya msimu ujao makadirio ya matumizi ni Tsh Bil 20.8 wakati mapati ni Tsh 14.8, uongozi wa Yanga umepewa jukumu kupitia vyanzo vingine kupata fedha kukamilisha bajeti



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz