Utovu wa nidhamu wamponza Lionel Messi - EDUSPORTSTZ

Latest

Utovu wa nidhamu wamponza Lionel Messi

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Nahodha wa Argentina Lionel Messi amesimamishwa kucheza katika kablu yake ya Paris St-Germain kwa wiki mbili baada ya kusafiri kwenda nchi ya Saudia Arabia bila ruhusa ya klabu hiyo wiki hii.


Safari yake ilifuatia kushindwa kwa klabu hiyo ya Ufaransa nyumbani na Lorient siku ya Jumapili, ambapo Messi alicheza kipindi chote cha dakika 90 za mechi.


Messi hatafanya mazoezi wala kuichezea PSG katika kipindi cha kusimamishwa kwake.


Inafahamika kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35 - aliomba ruhusa kufanya ya kusafiri ili kufanya kazi za kibiashara lakini alikataliwa.


Messi, ambaye pia alipigwa faini na klabu, ana kazi kama balozi wa utalii wa Saudi Arabia.


Mkataba wa mshindi huyo wa Kombe la Dunia na PSG unaisha msimu huu.


Makamu wa rais wa Barcelona Rafael Yuste alidai mwezi Machi kuwa klabu ya Uhispania inawasiliana na Messi kuhusu kurejea kwake katika Nou Camp.


Messi alifunga mabao 31 na kuchangia ushindi wa mabao 34 katika mechi 71 za mashindano yote ya PSG, na alishinda taji la Ligi 1 msimu uliopita.


Chanzo: Bbc



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz