Simba yatangaza dakika 180 za furaha - EDUSPORTSTZ

Latest

Simba yatangaza dakika 180 za furaha

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Baada ya mapumziko ya siku nne kumalizika, kikosi cha Simba kimerejea mazoezini ili kujiandaa na mechi mbili zilizobakia za Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Polisi Tanzania na Coastal, lakini pia maandalizi ya msimu mpya.


Mazoezi hayo yamefanyika kwenye Uwanja wa Mo Simba Arena, Bunju Dar es Salaam chini ya Kocha Mkuu, Robert Oliveira 'Robertinho’ ambaye alisema wachezaji wote wameshiriki programu hiyo.


Robertinho alisema anaimani mchezo ujao watavuna pointi tatu ili kumaliza ligi kwa heshima.


"Tunajiandaa vizuri kuhakikisha tunapata matokeo mazuri kwa kuvuna pointi sita ili kumaliza ligi kwa heshima na kuanza kujiandaa kwa msimu mpya," alisema kocha huyo.


Aliongeza anaimani na wachezaji wake watapambana kuhakikisha wanafanya vizuri katika michezo hiyo kwa lengo la kuwapa furaha wanachama na mashabiki wa klabu hiyo ambao waliwasapoti wakati wote.


Alisema pia mipango kuelekea msimu mpya imeshaanza na wanawaahidi mashabiki watawafuta machozi kutokana na kushindwa kufikia malengo msimu huu.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz