Chama anaamini Simba itarejesha makali msimu ujao - EDUSPORTSTZ

Latest

Chama anaamini Simba itarejesha makali msimu ujao

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Kiungo mshambuliaji wa Simba, Clatous Chama amesema haikuwa lengo kumaliza msimu huu pasipo kushinda taji lakini wamejifunza kutokana na makosa waliyofanya na msimu ujao utakuwa tofauti


Kinara huyo wa pasi za mabao katika ligi kuu ya NBC amesema wachezaji wamechukizwa kukosa kombe lolote katika msimu huu, watajipanga vizuri kuhakikisha wanabeba mataji yote ya ndani katika msimu ujao


"Zipo sababu nyingi zinazoweza kupelekea kukosa ubingwa timu yoyote ikakosa ubingwa kama ilivyokuwa kwetu, wakati mwingine sababu zinaweza kuwa nje au ndani ya uwanja"


"Tuwaambie mashabiki na wanachama wa Simba kuwa tutarejea msimu mwingine na zaidi kupambania ubingwa wa ligi na Kombe la ASFC, tunafahamu tulipokosea tutarejea tukiwa kamili kufanikisha malengo yetu"


"Hakuna kitakachoshindikana kwetu, zaidi ya sisi wachezaji wenyewe kufahamu sababu iliyopelekea kukosa makombe msimu huu," amesema Chama



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz