Ubaguzi wa rangi aliofanyiwa Lukaku waiponza Juventus - EDUSPORTSTZ

Latest

Ubaguzi wa rangi aliofanyiwa Lukaku waiponza Juventus

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Klabu ya Juventus imepewa adhabu ya kucheza mchezo mmoja bila sehemu ya jukwaa moja la mashabiki wao baada ya kumtusi kwa kejeli za kibaguzi mshambuliaji wa Inter Milan, Romelu Lukaku


Lukaku alilengwa na mashabiki wa Juventus kabla na baada ya kufunga penati dakika ya tano ya muda ulioongezwa na kuwafanya Inter kutoka sare ya bao 1-1 katika mechi ya mkondo wa kwanza ya nusu fainali ya Coppa Italia iliyochezwa Jumanne iliyopita


Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji alipewa kadi ya pili ya njano kwa kuweka vidole kwenye midomo yake ili kuwanyamazisha mashabiki kwenye Uwanja wa Allianz


Bodi ya Ligi Kuu Italia, Serie A, imetangaza Juve lazima wafunge jukwaa moja la Kusini kwa mchezo wao ujao wa ligi ya nyumbani, ambao ni dhidi ya Napoli utakaochezwa Aprili 23, mwaka huu


Lukaku bado atatumikia adhabu ya kufungiwa mechi moja katika mechi ya marudiano na Juve itakayochezwa Aprili 26, mwaka huu kwa kuonyeshwa kazi nyekundu.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz