Real Madrid waangukia pua mbele ya villareal - EDUSPORTSTZ

Latest

Real Madrid waangukia pua mbele ya villareal

 

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Matumaini ya Real Madrid ya kutwaa ubingwa wa La Liga yalipata pigo kubwa Jumamosi usiku huku mabao ya Samuel Chukwueze yakiipatia Villarreal ushindi wa mabao 3-2 kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu


Wenyeji walikuwa wametangulia kupata bao kupitia kwa Pau Torres lakini Chukwueze akafunga bao la kusawazisha


Bao pekee la Vinicius Jr liliiweka Real mbele lakini Jose Luis Morales akasawazisha kabla ya Chukwueze kuwashangaza wenyeji kwa bao la tatu


Huku kukiwa na mechi 10 tu za La Liga zilizosalia, Real ingehitaji kumaliza kwa nguvu msimu huu huku wakiomba Barcelona kuanguka ili kutetea ubingwa wao


Real walidhani walipata nafasi ya kusawazisha dakika za lala salama walipopewa penalti lakini baadae mwamuzi akabatilisha uamuzi wake baada ya ukaguzi wa VAR


Ushindi huo unaifanya Villarreal kupanda hadi nafasi ya tano kwenye msimamo, pointi nne kutoka kwenye nafasi nne za juu


Barcelona wanaweza kuongeza gap la pointi kufikia 15 kama watapata ushindi dhidi ya Girona siku ya Jumatatu



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz