Matokeo Sevilla vs Man United jana - EDUSPORTSTZ

Latest

Matokeo Sevilla vs Man United jana

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Safu ya ulinzi ya Manchester United imeendelea kuonyesha udhaifu mkubwa katika jitihada zao za kujijenga upya kufuatia makosa mengi katika mchezo wa mkondo wa pili robo fainali ya ligi ya Europa dhidi ya Sevilla


Man United ilitolewa kwenye mashindano hayo Jana usiku baada ya Sevilla kuwacharaza 3-0 na kuwaondosha kwa jumla ya mabao 5-2


Baada ya kuongoza kwa mabao 2-0 kabla ya mabao mawili ya kujifunga wenyewe mwishoni mwa mechi ya kwanza, Man United walikuwa na matumaini kwamba wangeweza kufika nusu fainali nyingine baada ya kushinda Kombe la Carabao na kutinga nusu fainali ya Kombe la FA


Lakini haikuwa hivyo, kwani makosa yao yaliwagharimu huku Youssef En-Nesyri na mchezaji wa zamani wa Nottingham Forest Loic Bade wakifunga mabao yaliyoipeleka Sevilla nusu fainali.


Baada ya kipigo hicho, mkufunzi wa Manchester United Erik ten Hag amekiri kuwa ipo changamoto katika safu yake ya ulinzi na kwa sasa ni lazima wakubali ili kupata ufumbuzi wa changamoto hiyo



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz