Kama unawachukulia Simba Poa, hivi ndivyo watakavyo pindua meza Morocco - EDUSPORTSTZ

Latest

Kama unawachukulia Simba Poa, hivi ndivyo watakavyo pindua meza Morocco

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Wydad Casablanca kwenye mechi ya robo fainali ya mkondo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Kocha Mkuu wa Simba, Robertinho Oliveira, amesema kazi bado haijamalizika na wataenda na sura mpya katika mchezo wa marudiano utakaopigwa Ijumaa nchini Morocco


Simba inatarajiwa kusafiri nchini Morocco kwa ajili ya mechi ya marudiano Aprili 28, mwaka huu katika Uwanja wa Mohammed V, kusaka ushindi ama sare yoyote ili kutinga nusu fainali


Robertinho amesema anatambua mchezo wa pili utakuwa tofauti hivyo ataandaa mkakati tofauti wa uchezaji ili kuhakikisha wanapata matokeo mazuri ambayo yatawavusha hatua inayofuata


"Haitakuwa mechi rahisi na tutalazimika kucheza kwa mbinu tofauti, na wachezaji kuingia kivingine katika mchezo wa marudiano tofauti na tulivyocheza nyumbani ili kufikia malengo yetu ya kusonga mbele kucheza nusu fainali," alisema Robertinho


Robertinho amesema anaimani kubwa na wachezaji aliokuwa nao ndani ya kikosi kuwa watafanikisha malengo yao 


Simba itacheza uwanja wa Mohammed V kwa mara ya pili msimu huu katika michuano ya ligi ya mabingwa


Mara ya mwisho walicheza na Raja Casablanca kwenye hatua ya makundi na kupoteza kwa kufungwa mabao 3-1



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz