Simba kuwafuata Raja Casablanca Kwa mafungu - EDUSPORTSTZ

Latest

Simba kuwafuata Raja Casablanca Kwa mafungu

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Msafara wa kikosi cha Simba unaondoka jijini Dar es salaam leo saa tisa Alasiri kuelekea Morocco kukamilisha hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Raja Casablanca


Taarifa iliyotolewa na Simba, imebainisha kuwa msafara huo utapitia Doha, Qatar na watawasili Morocco siku ya Jumatano asubuhi


Msafara utajumuisha wachezaji 13 huku nyota wengine ambao wako katika majukumu ya timu za Taifa wataungana na timu huko Morocco


Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema wachezaji saba hawatasafiri kutokana na sababu mbalimbali


Mohammed Hussein 'Zimbwe Jr' ana kadi mbili za njano wakati Jonas Mkude, Mohammed Mussa, Jimmyson Mwanuke na Ismail Sawadogo ni majeruhi huku Mohammed Ouattara akibaki kwa kukosa 'fitness'


Simba itachuana na Raja usiku wa kuamkia Jumamosi, April 01, saa 7 usiku



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz