Match day Live : Tanzania vs Uganda - EDUSPORTSTZ

Latest

Match day Live : Tanzania vs Uganda


 Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' leo inatupa karata muhimu kuwania tiketi ya kufuzu michuano ya Afcon 2023 kwa kuikabili Uganda katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa


Mtananange huo wa dabi ya Afrika Mashariki, utapigwa kuanzia saa 2 usiku


Huu ni mchezo muhimu kwa Tanzania kushinda ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu michuano ya Afcon 2023 ambayo itafanyika baadae mwaka huu huko Ivory coast


Ushindi kwa Stars dhidi ya Uganda leo utawafanya wafikishe alama saba hivyo kuhitaji alama moja tu katika mechi mbili zitakazokuwa zimebaki dhidi ya Niger na Algeria ili kufuzu


Jana Niger ilichapwa bao 1-0 na Algeria na hivyo kuwahakikisha Algeria kuwa timu ya kwanza kufuzu kwa michuano hiyo baada ya kufikisha alama tisa


Tanzania inashika nafasi ya pili ikiwa na alama nne, Niger ni wa tatu wakiwa na alama mbili wakati Uganda wanaburuza mkia wakiwa na alama moja katika kundi F


Stars inahitaji angalau alama nane tu kuweza kufuzu, alama tatu lazima zipatikane kwa Mkapa leo halafu kumaliza kazi hapohapo kwa Mkapa kwenye mchezo utakaofuata dhidi ya Niger mwezi Juni


Habari njema ni kuwa hakuna kiingilio kwa majukwaa ya Mzunguuko, mageti ya dimba la Mkapa yatafunguliwa kuanzia saa sita mchana


Kuwahi kwako uwanjani ndio tiketi yako kwani uwanja utakapokuwa umejaa, mageti yatafungwa!



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz