Mpaka Sasa Simba wamejihakikishia kupata kitita hichi Cha Fedha baada ya kutinga Robo Fainali ligi ya mabingwa - EDUSPORTSTZ

Latest

Mpaka Sasa Simba wamejihakikishia kupata kitita hichi Cha Fedha baada ya kutinga Robo Fainali ligi ya mabingwa

Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA

Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA
 

Klabu ya Simba imejihakikishia kuvuna Tsh Bilioni 1.5 kutoka kwa Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) baada ya kufanikiwa kutinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika


Juzi Simba ilitinga hatua hiyo kibabe kwa kuwafumua Horoya Ac mabao 7-0 katika moja ya vipigo vya kihistoria kwenye michuano ya ligi ya mabingwa


Simba inakuwa timu ya pili kushusha 'kipigo heavy' katika michuano hiyo TP Mazembe ikishikilia rekodi ya ushindi wa mabao 8-0 dhidi ya Club Africain


CAF iliongeza zawadi za fedha ambazo timu zitalipwa kila hatua kuanzia makundi mpaka bingwa wa mashindano


Kama Simba itafanikiwa kutinga nusu fainali itavuna takribani Tsh Bilioni 2 wakati ikitinga fainali itakuwa na uhakika wa kuvuna Tsh Bilioni 2.9 na kama itwaa ubingwa basi mipesa itakuwa mingi zaidi kufikia Tsh Bilioni 5.8



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz