Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA
Hiyo inafanya Yanga iwe na uhakika wa kuvuna takribani Tsh Bilioni 2.3 katika michuano hiyo hata kama itaishia hatua ya robo fainali
Yanga ina mkataba na kampuni ya Haier wenye thamani ya Tsh Bilioni 1.5 ambao ni maalum kwa ajili ya kombe la Shirikisho
Kama Wananchi watafanikiwa kutinga nusu fainali watavuna Tsh Bilioni 1 kutoka CAF (jumla Tsh Bil 2.5) na kama watatinga fainali watavuna Tsh Bil 1.5 (jumla Tsh Bilioni 3) na ikitokea wametwaa ubingwa wa Shirikisho Wananchi watavuna Tsh Bilioni 3 kutoka CAF na hivyo kukusanya jumla ya Tsh Bilioni 4.5 ikiwa ni pamoja na fedha za Haier
Pia kuna fedha za bonus kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dk Samia Suluhu Hassan mpaka sasa Yanga ikivuna Tsh Milioni 40 baada ya kufunga mabao nane
Kwa hakika huu utakuwa msimu bora kwa Yanga katika kukusanya mapato katika mashindano ya CAF
No comments:
Post a Comment