Hii hapa siku tarehe ya Yanga kuifuata Tp mazembe - EDUSPORTSTZ

Latest

Hii hapa siku tarehe ya Yanga kuifuata Tp mazembe


Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Klabu ya Yanga itaondoka nchini kesho Alhamisi kuelekea DR Congo ambako wanakabiliwa na mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya TP Mazembe


Mchezo huo wa kuhitimisha hatua ya makundi, utapigwa Jumapili, April 02 katika dimba la TP Mazembe, saa 10 jioni


Ni mechi muhimu kwa Yanga kusaka ushindi ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kumaliza kinara wa kundi D


Msafara wa Yanga utajumuisha Mashabiki ambao wanakwenda kuongeza hamasa leo ikiwa siku ya mwisho kujiandikisha zoezi likitarajiwa kufungwa saa 10 jioni


Meneja wa masuala ya Digitali, Priva Abiudi Shayo 'Privaldinho' amesema wakiwa DR Congo wanatarajiwa kuzindua tawi rasmi la klabu hiyo katika Mji wa Lubumbashi


Zaidi ya Wananchi 50 kutoka DR Congo wamejiandikisha kuwa Wanachama wa Yanga ambapo Privaldinho amesema watakabidhiwa kadi zao kwenye hafla ya uzinduzi wa Tawi hilo


Msafara wa Mashabiki wa Yanga unatarajiwa kuondoka jijini Dar es salaam kesho Alhamisi kuelekea DR Congo ambapo watakuwa huko kwa siku tatu, timu itarejea nchini April 03 baada ya mchezo dhidi ya TP Mazembe



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz