KIINGILIO TAIFA STARS NA ALGERIA NI SH 3,000 KESHO DAR-Michezoni leo - EDUSPORTSTZ

Latest

KIINGILIO TAIFA STARS NA ALGERIA NI SH 3,000 KESHO DAR-Michezoni leo

Pakua App ya 'EDUSPORTSTZ NEWS' Uweze kufurahia Habari zote za Mapenzi; Udaku, Ajira na Michezo kila siku Ipo Google Playstore, Kwa Ku BONYEZA INSTALL Ili KUIDOWNLOAD Kwenye Simu yako nakutasoma habari zote hata kama hauna MB

KIINGILIO cha chini katika mchezo wa Kundi F kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwakani nchini Ivory Coast baina ya wenyeji, Tanzania na Algeria ni Sh. 3,000.
Bei hiyo ni kwa majukwaa ya mzunguko, wakati kwa VIP A, B na C ni Sh. 5,000.
Ikumbukwe mechi za kwanza za kuwania tiketi ya Ivory Coast, wakiwa nyumbani Jijini Algiers, Algeria waliichapa Uganda 2-0 na Taifa Stars wakiwa ugenini Jijini Cotonou nchini Benin, walitoa sare ya 1-1 na Niger.
Mbali na Stars na Algeria kumenyana kesho Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam, jirani zao, Uganda watakuwa wenyeji wa Niger Jijini Kampala.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz