Ukraine yajingamba Kufanikiwa Mashambulizi dhidi Urusi. - EDUSPORTSTZ

Latest

Ukraine yajingamba Kufanikiwa Mashambulizi dhidi Urusi.




Jeshi la Ukraine limedai kufanikiwa mashambulizi na kikosi chake cha ndege zisizo na rubani kilichoundwa na Uturuki dhidi ya vikosi vya Urusi.

Siku ya jumapili vikosi vya Wanajeshi vya Ukraine vilitoa picha zinazoonyesha uharibifu wa silaha na ndege isiyo na rubani na kusema kuwa ilitekelezwa dhidi ya mfumo wa makombora wa kutoka ardhini hadi angani wa BUK.

Valerii Zaluzhnyi Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Wanajeshi alisema shambulio hilo la ndege isiyo na rubani lilifanyika karibu na mji wa Malyn, kilomita 100 kaskazini magharibi mwa Kyiv.

#CNN




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz