Mvulana wa Kidato cha Nne Auawa Baada ya Kufumaniwa Akimtafuna Mke wa Wenyewe - EDUSPORTSTZ

Latest

Mvulana wa Kidato cha Nne Auawa Baada ya Kufumaniwa Akimtafuna Mke wa Wenyewe



Mwanafunzi huyo alikatwakatwa vipande kwa panga na mume wa mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 35
Akithibitisha kisa hicho, DCIO wa Kuresoi Peter Obonyo alisema mwanafunzi huyo alifariki dunia akipokea matibabu katika hospitali ya Nakuru Level Five
Polisi wameanzisha msako dhidi ya mshukiwa kwa jina la Japheth Bii ambaye anasemekana aliingia mafichoni baada ya kisa hicho cha kusikitisha
Mwanafunzi wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Kapsumbeiywo huko Kuresoi Kusini, Kaunti ya Nakuru aliuawa baada ya kupatikana na mwanamke wa wenyewe.

Mtahiniwa wa Kidato Cha Nne Auawa Baada ya Kufumaniwa na Mke wa Wenyewe
Mtahiniwa wa kidato cha Nne aliuwawa baada ya kufumaniwa na mke wa wenyewe. Picha: Getty Images.
Mwanafunzi huyo alikatwakatwa vipande kwa panga na mume wa mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 35.

Akithibitisha kisa hicho, DCIO wa Kuresoi Peter Obonyo alisema mwanafunzi huyo alifariki dunia akipokea matibabu katika hospitali ya Nakuru Level Five.

Polisi wameanzisha msako dhidi ya mshukiwa huyo kwa jina kwa jina Japheth Bii ambaye anasemekana aliingia mafichoni baada ya kisa hicho cha kusikitisha.


 
Kwingineko jamaa mmoja alipoteza maisha yake baada ya kushambuliwa kwa kisu na mwenzake aliyempata katika boma lake eneo la Kagoto, kaunti ya Nakuru.

Maafisa wa polisi katika uchunguzi wao walisema kwamba kisa hicho kilitokea baada ya mshukiwa kupandishwa hasira na marehemu.

Vurugu hizo zilianza wakati Micah Nyaberi Bogomba aliporudi kwake ghafla saa tisa usiku Jumamosi, Agosti 28 na kumkuta jamaa huyo mwenye umri wa miaka 34 akijistarehesha kwake.


Nyaberi, mwenye umri wa miaka 39, alikuwa na hasira na alitaka kujua ni biashara gani haswa ilikuwa inaendelea kati ya Boniface Njagi Maina na mkewe Harriet Vivian Mboga.

Kabla ya mwenda zake kutamka lolote, mshukiwa alimrukia kwa ngumi nzito na mateke.

Kulingana na mashuhuda, Njagi ambaye alikuwa akihofia maisha yake aliripotiwa kumsihi Nyaberi amruhusu achukue viatu vyake na kuondoka, lakini ombi lake liliambulia patupu kwani alidungwa kisu begani.

Polisi kutoka Kituo cha Doria cha Kagoto walifika mara moja eneo la tukio na kuupata mwili wa Njagi ukiwa umelala kwenye damu iliyotapakaa katika lango la boma hilo. Katika nyumba ya mtuhumiwa, polisi pia walipata damu kwenye kuta na vifaa vya nyumbani, ambavyo vitatumika kwa ushahidi.


 
Washukiwa wawili Micah Nyaberi Bogomba na Harriet Vivian Mboga Musumba walikamatwa na kukabidhiwa kwa maafisa wa upelelezi wa DCI Nakuru Kaskazini ili wachukuliwe hatua za kisheria.

Mwili wa mwenda zake ulipelekwa katika makafani moja ya eneo hilo.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz