Askofu wa Kanisa Katoliki ajiuzulu sababu ya kupagawishwa na mapenzi - EDUSPORTSTZ

Latest

Askofu wa Kanisa Katoliki ajiuzulu sababu ya kupagawishwa na mapenzi




 
Askofu Xavier Novell alipojiuzulu mnamo Agosti 2021, Kanisa Katoliki lilisema uamuzi wake ulitokana na sababu za binafsi
Vyombo vya habari nchini Uhispania vilifichua kuwa sababu za Novell kuacha kazi ni kutokana na kumpenda mama wa watoto wawili aliyetalakiana na mume wake
Mama huyo ni mwanasaikolijia na mwandishi wa vitabu vya simulizi vyenye maudhui ya "kishetani" jambo ambalo limewashangaza wengi
Askofu wa Kanisa Katoliki kutoka nchini Uhispania amejiuzulu kwa sababu ya kupagawishwa na mapenzi ya mwanamke mmoja mwandishi wa simulizi za kusadikika.

Mapenzi Yamzingua Askofu wa Kanisa Katoliki na Kumfanya Kuacha Kazi
Askofu Xavier Novell anadaiwa kuacha kazi kutokana na kumpenda Silvia Caballol.Picha:The Guardian.
Wakati Askofu Xavier Novell mwenye umri wa miaka 52, alijiuzulu mnamo Agosti 2021, Kanisa Katoliki lilisema uamuzi wake ulitokana na sababu za binafsi.

Hata hivyo, mnamo Jumatatu, Septemba 6, vyombo vya habari nchini Uhispania vilifichua kuwa sababu za Novell kuacha kazi ni kutokana na kumpenda Silvia Caballol, ambaye ni mama wa watoto wawili aliyetalakiana na mume wake.

Caballol,38, alikuwa mwanasaikolijia na mwandishi wa vitabu vya simulizi vyenye maudhui ya "kishetani" jambo ambalo limewashangaza wengi.


 
Aliyekuwa Muigizaji Katika Kipindi cha Gumbaru School Mzee Mathiokore Ameaga Dunia
Askofu huyo alipata umaarufu katika Kanisa Katoliki la Uhispania mwaka 2010, baada ya kuteuliwa akiwa na umri wa miaka 41, na kuwa askofu mdogo zaidi kaskazini mashariki mwa mji wa Catalonia

Novell pia alishangaza wengi kwa kuunga mkono kile kinachoitwa tiba ya uongofu kwa watu wenye mapenzi ya jinsia moja na kutoa mapepo.

Askofu huyo alipenda sana kuzungumzia kuhusu uavyaji mimba na kutoa maoni makali kuhusu mapenzi ya jinsia moja.


Uamuzi wake wa kujiuzulu uliidhinishwa na kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis lakini bado kanisa hilo halijatoa taarifa kuhusu kujiuzulu kwake.

Duru zinaarifu kuwa askofu huyo wa zamani sasa anatafuta ajira katika eneo la Barcelona kama mtaalamu wa kilimo.

Padri awabusu wanafunzi wa kike madhabauni
Tuko.co.ke iliripotia awali kuhusu kisa kimoja ambapo video ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii kama moto ikimuonyesha kiongozi wa kidini akiwabusu wanafunzi watatu wa kike kwenye mimbari.

Padri huyo ambaye anasemekana kuwa wa Kanisa la Anglikana nchini Ghana, anaonyeshwa akiwa amevalia nguo za kijani, kisha aliwaita wanafunzi hao kwenye mimbari, akawavua barakoa zao kabla ya kuwabusu.


 
Mama Aliyezaa Mtoto Mwenye Ugonjwa wa Kuzeeka Haraka Aomba Serikali Imchukuwe
Source: Tuko




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz