Polisi akosa la kufanya baada ya kupokonywa simu na mtu aliyekuwa kwenye pikipiki - EDUSPORTSTZ

Latest

Polisi akosa la kufanya baada ya kupokonywa simu na mtu aliyekuwa kwenye pikipiki



Video ya polisi wa usalama barabarani katika mji mkuu wa Kenya Nairobi, akiibiwa siku yake ya mkononi na wanaume watatu waliokuwa kwenye pikipiki imekuwa ikisambazwa sana kwenye mitandao ya kijami.

Picha ya video hiyo iliyorekodiwa na dashcam, sinamuonesha afisa huyo akizungumza kwa simu yake kabla ya mwendesha pikipiki kupita na abiria ambaye alinyakua simu kutoka kwa polisi.

Wanaume hao wawili walitoweka kwenye msururu wa magari na kumuacha polisi akionekana hana la kufanya.

Haijawa wazi ni wapi hasa video ya tukio hilo ilichukuliwa ,lakini video inaonesha ilichukuliwa mwezi wa Julai.

Unyakuaji wa simu za mkononi, mikoba na vipuli unaofanywa na wezi wanaotumia pikipiki umekithiri jijini Nairobi.

Maafisa wamekuwa wakiwaonya watu kuwa macho wakati wanapotembea kwenye mitaa ya jiji la Nairobi.

Uhalifu kama vile ujambazi na utekaji nyarapia umeongezeka wiki huku polisi wiki hii wakitangaza kuunda kikosi maalum cha kukabiliana na uhalifu huu.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz