Mkasa wa wanandoa. MKE WANGU HAJUI, KWAMBA MIMI NAJUA. - EDUSPORTSTZ

Latest

Mkasa wa wanandoa. MKE WANGU HAJUI, KWAMBA MIMI NAJUA.


Nimekuwa kwenye ndoa kwa miaka 14, na tuna watoto 3, wote wanaume, lakini hakuna ata mmoja ambaye ni damu yangu. Najua ili kwa uhakika kabisa, lakini mke wangu hajui kwamba Mimi najua.
NGOJA NIWASIMULIE......
Miaka 5 kabla yakukutana na mke wangu, nilipatwa na ajali ya gari nikiwa pamoja na rafiki zangu wawili. Gari yetu iliaribika vibaya sana, nilipona peke yangu katika iyo ajali, nilitumia miezi 11 katika hospital moja hapa Dar, na mwisho kabisa niliambiwa siwezi kupata Mtoto tena katika maisha yangu.
Niliamua kumpa YESU maisha yangu (kuokoka) na nikatubu dhambi zangu huku nkimshukuru MUNGU kwa kuniokoa na ile ajali ambayo imewachukua rafiki zangu wawili.
Baada muda nikawa mchungaji katika kanisa dogo la mtaani kwangu,miaka 5 baadaye ndio nikakutana na mke wangu tukiwa katika moja ya mikutano ya injili. Sikumweleza juu ya hali yangu, kwasababu nilikuwa na matumaini kwamba MUNGU ataniponya.
Mwaka wa 6 yani ndio tukiwa na mwaka 1 ndani ya ndoa yetu, mke wangu alishika mimba kisha tukapata Mtoto wa kwanza.
Ili nipate uhakika, kwa siri nikaenda kupima DNA ikaonyesha wazi kabisa kuwa sikuwa Baba wa yule Mtoto. Sikumwambie, ajabu alishika tena mimba, mpaka akafikisha watoti 3, na Mimi kazi yangu ilikuwa nikupima tu kimwa kimya. Nilimlilia MUNGU anipe majibu sahihi, ivyo nikarudia tena kupima vipimo vya watoto wote 3, na wote hawakuwa wangu.
Niliishi na hii hali kwa miaka 8 nikaanza kuathiriwa na wote yani mama na watoto.
Kilichokuwa kikiniathiri zaidi ni pale ambapo mkewangu anaigiza kwa kujifanya mke mzuri na mwaminifu hapo ndio niliumia zaidi. Alikuwa akifanya makongamano kanisani nakuwashauri mabinti jinsi yakuishi maisha matakatifu yakumpendeza MUNGU na waume zao huku yeye ana watoto watatu na mwanaume au wanaume wangine ata sijui.
Nilitaka kumthibishia, lakini nilijiuliza itakuwaje baada ya hapo na Mimi ni Mtumishi wa MUNGU naye tazamwa na wengi.
Basi nikawa mwenye hasira na nisiyevutiwa na yoyote ndani ya nyumba yangu. Ni nikawa nahisi kama wote ni wageni tu ambao wameletwa na Shetani katika nyumba yangu.
Nifanye nini Mimi!?
Naomba unipe jibu lenye hekima ya MUNGU, maana kwa sasa siwezi ata kuomba wala kusimama mazabauni kuhubiri. Ajabu mke wangu yeye hajashtuka, ndio anazidi kujifanya anaupendo wa dhati kwangu.
KAMA MAJARIBU NI MTAJI BASI MUNGU ANISAIDIE NILISHINDE ILI JARIBU.
Share, uenda mkewangu akaiona nione atashauri nini.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz