CHUKUA HII KUHUSU MAFANIKIO ITAKUSAIDIA: - EDUSPORTSTZ

Latest

CHUKUA HII KUHUSU MAFANIKIO ITAKUSAIDIA:


🗨Tunakwama Wapi Kwenye Mafanikio??!
💨Muda huu baadhi ya watu wengine wamelala wanaota mafanikio, wakati wengine wameshaamka wanafanya kazi.
💨Yakupasa ujue mafanikio sio vitu ulivyokamilisha kwenye maisha yako, bali ni nini ulichowahamasisha wengine kufanya na wakafanikiwa kupitia wewe.
💨Mtu mwenye mafanikio ni yule anayeweza kujenga msingi imara kwa kutumia matofali mabovu yaliyotupwa na watu wengine.
💨Njia mbaya ya kufanikiwa ni pale unapojaribu kutafuta mtu ambaye ana furaha kwaajili yako.
💨Usijaribu kuwa mtu mwenye mafanikio, bali jaribu kuwa mtu wa thamani kwa thamani hukupa mafanikio.
💨Hakuna siri nyingine ya mafanikio, bali ni matokeo ya maandalizi, kufanya kazi kwa bidii na kujifunza kutokana na kushindwa.
💨Mafanikio ni kupita kutoka aina moja ya kushindwa hadi nyingine bila kukata tamaa.
💨Tuhitimishe hivi Mafanikio ni kupata unachotaka, furaha ni kutaka unachopata.
Okota hata moja Itakusaidia.............💥




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz