![Image may contain: 1 person](https://scontent-mrs2-1.xx.fbcdn.net/v/t1.0-9/15317774_1390565594296159_8193574780422907207_n.jpg?_nc_cat=111&_nc_sid=2d5d41&_nc_eui2=AeH7-9OBXLe9sY2QlApMgZgagK47N_jeLXwG-PYY9juO53s7Es4EkhkOVNQLyqBZLXRhldcarMdfpXSbGR1Xcv_j6t8tJDuuYrhhx9L3y5reiA&_nc_ohc=LKvz1U8uQI8AX_5qDib&_nc_ht=scontent-mrs2-1.xx&oh=f9dec0f970041b25d8ea5ca5906ae5ff&oe=5E91FE2C)
...... _Kuna mambo madogo madogo ambayo unatakiwa kumfanyia mkeo kila siku ili kuufanya uhusiano wenu uendelee kuwa hai._
...... _Yanaweza kuwa madogo lakini yanaleta tofauti kubwa sana. Ifuatayo ni orodha ya mambo 10 unayoweza kumfanyia kila siku:_
💖💖💖💖💖💖💖💖💖
*1. Wapende watoto wake:*
...... _Kama mna watoto, hakuna kitakachomfurahisha sana kama kukuona kama baba mwenye upendo._
💞💞💞💞💞💞💞💞💞
*2. Mbusu:*
...... _Kila unapotoka na kuingia nyumbani, mbusu. Hakika busu linatuma ujumbe maridhawa kwenye moyo wake._
💖💖💖💖💖💖💖💖💖
*3. Mkumbatie:*
...... _Kumbatio huwaweka karibu na humfanya ajihisi amani na kuwa na hisia ya kupendwa. Inapendekezwa kuwa umguse mkeo angalau mara 31 kwa siku._
💞💞💞💞💞💞💞💞💞
*4. Mpe sifa ya kipekee:*
...... _Kuna vitu vingi vya kuvutia kuhusu mkeo. Kila siku tafuta kitu kipya na umwambie kuhusu kitu hicho. Mpambe na umsifu._
💖💖💖💖💖💖💖💖💖
*5. Mchokoze:*
...... _Wakati fulani mkeo anahitaji kukumbushwa kuwa anatakiwa kuwa laini na asiyekuwa na ugumu; anahitaji kutaniwa, kuchokozwa na kuchekeshwa._
💞💞💞💞💞💞💞💞💞
*6. Mfanye ajisikie kuwa yu salama:*
...... _Fungeni milango na umbebe, hasa kama nje kuna watu au kuna kelele zinazowanyima utulivu._
💖💖💖💖💖💖💖💖💖
*7. Zima simu yako:*
...... _Tenga muda angalau kidogo wakati wa usiku na ukae na mkeo badala ya simu yako._
💞💞💞💞💞💞💞💞💞
*8. Muombee dua:*
...... _Kila siku katika sala na maombi yako, usimsahau mkeo… muombee kwa Allaah ._
💖💖💖💖💖💖💖💖💖
*9. Mchekeshe:*
...... _Kama unaweza kumchekesha kila siku, mtaweza kukabiliana na chochote._
💞💞💞💞💞💞💞💞💞
*10. Mwambie*
*“Ninakupenda”:*
...... _Kila siku litamke neno hilo, hatochoka kulisikia na kulisikiliza._
💞💖💞💖💞💖💞💖💞💖💞💖💞💖💞💖💞💖 💞 *MAFUNZO YA NDOA* 💞💖💞💖💞💖💞💖💞💖💞💞💖💞💖💞💖💖💞
No comments:
Post a Comment