*MAMBO 10 YA KUMFANYIA MKEO KILA SIKU* - EDUSPORTSTZ

Latest

*MAMBO 10 YA KUMFANYIA MKEO KILA SIKU*

Image may contain: 1 person

...... _Kuna mambo madogo madogo ambayo unatakiwa kumfanyia mkeo kila siku ili kuufanya uhusiano wenu uendelee kuwa hai._

...... _Yanaweza kuwa madogo lakini yanaleta tofauti kubwa sana. Ifuatayo ni orodha ya mambo 10 unayoweza kumfanyia kila siku:_

💖💖💖💖💖💖💖💖💖
*1. Wapende watoto wake:*

...... _Kama mna watoto, hakuna kitakachomfurahisha sana kama kukuona kama baba mwenye upendo._

💞💞💞💞💞💞💞💞💞
*2. Mbusu:*

...... _Kila unapotoka na kuingia nyumbani, mbusu. Hakika busu linatuma ujumbe maridhawa kwenye moyo wake._

💖💖💖💖💖💖💖💖💖
*3. Mkumbatie:*

...... _Kumbatio huwaweka karibu na humfanya ajihisi amani na kuwa na hisia ya kupendwa. Inapendekezwa kuwa umguse mkeo angalau mara 31 kwa siku._

💞💞💞💞💞💞💞💞💞
*4. Mpe sifa ya kipekee:*

...... _Kuna vitu vingi vya kuvutia kuhusu mkeo. Kila siku tafuta kitu kipya na umwambie kuhusu kitu hicho. Mpambe na umsifu._

💖💖💖💖💖💖💖💖💖
*5. Mchokoze:*

...... _Wakati fulani mkeo anahitaji kukumbushwa kuwa anatakiwa kuwa laini na asiyekuwa na ugumu; anahitaji kutaniwa, kuchokozwa na kuchekeshwa._

💞💞💞💞💞💞💞💞💞
*6. Mfanye ajisikie kuwa yu salama:*

...... _Fungeni milango na umbebe, hasa kama nje kuna watu au kuna kelele zinazowanyima utulivu._

💖💖💖💖💖💖💖💖💖
*7. Zima simu yako:*

...... _Tenga muda angalau kidogo wakati wa usiku na ukae na mkeo badala ya simu yako._

💞💞💞💞💞💞💞💞💞
*8. Muombee dua:*

...... _Kila siku katika sala na maombi yako, usimsahau mkeo… muombee kwa Allaah ._

💖💖💖💖💖💖💖💖💖
*9. Mchekeshe:*

...... _Kama unaweza kumchekesha kila siku, mtaweza kukabiliana na chochote._

💞💞💞💞💞💞💞💞💞
*10. Mwambie*

*“Ninakupenda”:*
...... _Kila siku litamke neno hilo, hatochoka kulisikia na kulisikiliza._

💞💖💞💖💞💖💞💖💞💖💞💖💞💖💞💖💞💖 💞 *MAFUNZO YA NDOA* 💞💖💞💖💞💖💞💖💞💖💞💞💖💞💖💞💖💖💞




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz