KINACHOTESA MOYO BAADA YA MAPENZI KUINGILIWA NA DOSARI NI......! - EDUSPORTSTZ

Latest

KINACHOTESA MOYO BAADA YA MAPENZI KUINGILIWA NA DOSARI NI......!

Unhappy couple not speaking to each other on sofa at home in the living room Stock Photo - 30979581

KUINGILIWA NA DOSARI ni pale mtu unapokuwa umechoka matendo mabaya ya mwenza wako na ukililia mabadiliko lakini mwenzio hajari, Moyo una tabia ya kujitetea kwa kutaka kuachana na MAPENZI lakini MOYO huo huo ni mwoga kuacha... Mbaya zaidi ni pale unapokuwa umeamua kuacha/kuondoka kwa kutumia akili shida inakuja kama unakokwenda MOYO HAUJARIDHIA! Vita ya MOYO NA AKILI hichukuwa kasi pale ulipokwenda hakuna tofauti na ulikotoka, Yaani MOYO hulalamikia AKILI kutaka kudhurumu PENDO lake... AKILI nayo kuulalamikia MOYO kushindwa kuchukuwa maamuzi wakati AKILI ndo mhanga wa kufikiri, Hapo ndipo utabaini kwamba MOYO NDO WENYE DHAMANA YA KUENDELEA AMA KUACHA MAPENZI! Uonapo unashindwa kuamua jambo linalohusu MAPENZI basi mtafute hata mmoja kati ya wazazi wako mpe siri ya PENZI ulilopo japo uweze kupata nafuu ya NYAKATI NGUMU ULIZOPO... Yaliitwa MAPENZI ili kuleta FURAHA MOYONI lakini uonapo hauko kwenye MAPENZI YENYE FURAHA ukunjue moyo wako ili uweze kushirikiana na akili katika kupokea tatizo lililoko mbele yako, Bin adam awaye yeyote hapendi kuumizwa IWEJE UNAVUMILIA MAUMIVU KWA MTU AMBAYE YEYE MWENYEWE HAPENDI KUUMIA? Ukiona nakuingilia kwenye mambo ya NAFSI yako potezea, Elista akisema haimaanishi ufanyie kazi alilosema bali ANAKUFUNGUA AKILI japo ujisogeze kwenye kufikiria hilo linalokutesa.
#Elista_kasema_ila_sio_sheria ðŸ’‰ðŸ’ŠðŸ‘Œ




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz