HIZI NDIZO TABIA ZETU WANAWAKE KWA WAPENZI/WAUME ZETU,AMBAZO WAO HUZIONA KERO...... - EDUSPORTSTZ

Latest

HIZI NDIZO TABIA ZETU WANAWAKE KWA WAPENZI/WAUME ZETU,AMBAZO WAO HUZIONA KERO......

Image result for MAISHA YA UPENDO YA MUME & MKE YANAJIONYESHA KWA MAMBO YAFUATAYO
Mwanamke akikupenda atakukera kwa wivu wake, na vijiswali swali vyake ambavyo wewe utaviona vya kijinga "Huyu nani? Kwanini unachat nae sana".
Usimuone mjinga, usimuone kero kwako. Sio kosa lake, tatizo moyo wake huwa dhaifu pindi anapopenda na ngumu kuzizuia hisia zake.
Atakuchunga, atakulinda, atakukagua kila kona hata comment zako za Facebook na Instagram.
Usimkaripie na kumuona kama hana kazi ya maana ya kufanya.
Muache afanye kazi ya kukulinda, hiyo ni haki yake.
Yuko hivyo, anapenda kuhakikisha mpenzi wake yuko salama wakati wote.
Na usiombee akiwa ana wasiwasi juu ya jambo lolote kati yako na mwanamke mwengine.
Atakupeleleza mpaka apate majibu kamili ya yale aliyokuwa na wasiwasi nayo.
Tuko hivyo...
lakini hutakiwi kumchukia, sababu kukuonyesha wivu ni haki yake ya msingi.
Na unatakiwa kujivunia unapendwa, sababu angekuwa hakupendi, wala usingemuona akihangaika kufanya yote hayo.
#Mjue_Mwanamke_Wako
#usihukumu_usije_hukumiwa




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz