HII HAPA TAARIFA YA KIFO CHA MASOGANGE NA WASIFU WAKE - EDUSPORTSTZ

Latest

HII HAPA TAARIFA YA KIFO CHA MASOGANGE NA WASIFU WAKE

Agnes Masogange 

Taarifa zilizotufikia hivi punde ndani ya www.edusportstz.com zinadhibitisha kwamba Video Vixen maarufu nchini Agness Masogange amefariki dunia mchana huu wa leo April 20, 2018.

Chanzo cha kifo hiko ni baada ya presha kupanda ghafla mpaka kupelekea kulazwa hospitali na kufariki.

Kifo chake kimetokea katika hospitali ya Kwa Mama Ngoma iliyopo mwenge jijini Dar es Salaam aliokuwa anapatiwa matibabu.

Masogange alizaliwa tarehe 8, September mwaka 1989, akiwa na miaka 20s alijishughulisha na maswara ya urembo akiwa Kama video vixen na alimewahi kuchukua tuzo ya wanavideo vixen bora nchi kwa mwaka 2009, 2011, 2012.

Masongange alijipatia umaarufu kupitia kibao Chake bele9 kiitwacho "masogange" kilichitamba miaka ya 2011-2012

Awali mwa mwezi wa nne masogange alipatikana na hatia ya matumizi ya madawa ya kukevya Aina ya Heroin na Oxazepam.  Hukumu hiyo ilimtaka atoe faini ya 1.5Million au kifungo cha miaka 3. Masogange alitoa kiasi hicho na kuachiwa huru mnaomo tarehe 03 April mwaka huu.

Edusportstz inatoa pole kwa wafiwa wote na familia ya marehemu 


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz