MSIMAMO WA MANARA KUHUSU UZALENDO KWA KLABU ZA NDANI - EDUSPORTSTZ

Latest

MSIMAMO WA MANARA KUHUSU UZALENDO KWA KLABU ZA NDANI

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba, Haji Manara


Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba, Haji Manara, amesema hatoweza kuonesha uzalendo wa soka kwa ngazi ya klabu labda mambo mengine yasiyohusiana na soka.

Akizungumza na kipindi cha Sports Hedikota kinachorushwa na Radio EFM, Manara amesema hawezi kujitolea kuishabikia Yanga hata siku moja pale inaposhiriki mashindano ya kimataifa.

Manara ameeleza kuwa aliwahi kuhamasisha timu za Tanzania kuonesha uzalendo haswa pale klabu zinaposhiriki mashindano ya kimataifa, lakini akapuuzwa na viongozi wa Yanga.

Kutokana na kuupuzwa, Haji ameweka wazi kutothubutu tena kusapoti suala hili kutokana kutoungwa mkono na baadhi ya watu.

"Haitowezekana kamwe nikaonesha uzalendo kwa klabu za Tanzania, juzi hapa niliwaomba watu tuungane tuwe kitu kimoja lakini kuna mtu mmoja kutoka upande wa pili akanijibu kwa kebehi" alisema Manara.

EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati.
Enter your email address:


Delivered by EDUSPORTSTZ
Subscribe to EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz