VIWANJA VITAKAVYOTUMIKA FAINALI AFCON TANZANIA MWAKANI - EDUSPORTSTZ

Latest

VIWANJA VITAKAVYOTUMIKA FAINALI AFCON TANZANIA MWAKANI


Image result for AZAM COMPLEX

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe ametaja viwanja vitakavyotumika katika mashindano ya vijana chini ya miaka 17 katika fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) mwakani.


Waziri Mwakyembe alisema Uwanja wa Taifa utatumika kwaajili ya ufunguzi na kufungukia mashindano hayo, huku viwanja vingine vya Uhuru na Azam Complex Chamazi vikitumika katika mechi za mashindano hayo.

"Tunataka tufanye mabadiliko katika hizi nyasi bandia za uhuru tuweke mpya, lakini uwanja wa Gymkhana utatumika kwa mazoezi, bado kuna viwanja vingine tunaendelea kuvichagua ili timu zipate sehemu ya kufanyia mazoezi kwa urahisi," alisema Mwakyembe.

Waziri Mwakyembe alisema wanajua wingi wa timu nane zinazokuja zitakuwa na viongozi, wachezaji na mashabiki hivyo wanajiandaa kuhakikisha wageni hao wanapata mahitaji yao mapema.

"Magari yanahitajika kwaajili ya kuwabeba wageni wetu hivyo inabidi yapatikane na kuandaliwa mapema, lakini pia tunajupanga juu ya suala la foleni wasiweze kukutana nalo,'' alisema.

Mwakyembe aliongeza kwamba wanaendelea na maandalizi, wapo katika hatua nzuri kwa ajili ya mashindano hayo.

EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati.
Enter your email address:


Delivered by EDUSPORTSTZ
Subscribe to EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz