ZIJUE SABABU ZITAKAZOWAFANYA MASTAA AWA KUKOSA MECHI KATI YA YANGA NA MWADUI FC - EDUSPORTSTZ

Latest

ZIJUE SABABU ZITAKAZOWAFANYA MASTAA AWA KUKOSA MECHI KATI YA YANGA NA MWADUI FC


Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania Bara Yanga wanaendelea kuwakosa nyota wao muhimu kuelekea mchezo wao wa kesho dhidi ya Mwadui FC.

Akiongea leo mbele ya wanahabari msemaji wa timu hiyo Dismas Ten amesema wachezaji watakao kosekana katika mchezo huo ni Donald Ngoma, Geofrey Mwashiuya, Thabaan Kamusoko na Obrey Chirwa.

"Tunawachezaji wetu ambao bado ni wagonjwa na wataukosa mchezo wa kesho dhidi ya Mwadui huku Chirwa atakosekana kwasababu anatumikia adhabu ya kukosa mechi tatu aliyopewa na kamati ya maadili ya TFF'', amesema Ten.

Kwa upande wa mshambuliaji raia wa Burundi Amissi Tambwe, Ten amesema mchezaji huyo amepona Malaria iliyokuwa inamsumbua hivyo kinachosubiriwa ni uamuzi wa Mwalimu kama atampanga kesho.

Yanga inashika nafasi ya tano kwenye msimamo wa ligi ikiwa na alama 21. Mchezo huo wa kesho utachezwa saa 10:00 jioni kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati. 

BOFYA HAPA KUJIUNGA NA INNOVATION FURSA CHALLENGE http://www.edusportstz.com ni fahari ya wasomaji
UNGANA NASI KUPITIA LIKI HIZI ILI KUTUMIWA HABARI POPOTE ULIPO

EDUSPORTSTZ NI FAHARI YA WASOMAJI

WEKA EMAIL YAKO:


Delivered by EDUSPOTSTZ
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno
EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz