MSHAHARA WA KOCHA MPYA WA SIMBA WAIBUA MASWALI KIBAO UNGANA NA MCHAMBUZI WETU - EDUSPORTSTZ

Latest

MSHAHARA WA KOCHA MPYA WA SIMBA WAIBUA MASWALI KIBAO UNGANA NA MCHAMBUZI WETU



NDG MSOMAJI WA EDUSPORTSTZ UNAKUMBUSHWA KUSUBSCRIBE NA KUFOLLOW WEB YETU PAMOJA NA MITANDAO YETU YA KIJAMII CHINI YA POSITI HII ILI KUTUMIWA UPDATES ZOTE ZA AJIRA, MICHEZO, HABARI, SCHOLARSHIPS PAMOJA NA MASTORI YA MASTAA NA VIONGOZI MBALIMBALI. EDUSPOTSTZ NI FAHARI YA WASOMAJI.
KUANZIA jana mapema kulikuwa na mjadala mkubwa kuhusiana na suala la mshahara wa Kocha mpya wa Simba, Pierre Georges Lechantre.

Taarifa nilizozipata kwamba mshahara wake “ulivuja” na gazeti moja (si Championi wala Spoti Xtra), likaandika kwamba kocha huyo kila dakika analipwa Sh 42,000!

Kwa hasebu za kawaida kabisa ambazo hazitaki hata kuumiza kichwa, lazima kwa kocha huyo utaanza kumpigia kuzikuza kwenda kuutafuta mwezi.


Kocha huyo Mfaransa ni mwajiriwa wa Simba, unajua malipo yanakuwa ni ya mwezi. Hata yakiwa ya wiki, huwa yanatengenezwa kujenga mwezi.


Kuupata mwezi, lazima Sh 42,000 ya dakika uitafutie saa ambayo inakuwa ni mara 60, unapata Sh 2,520,000 (maana yake kocha huyu, kwa saa moja tu, mshahara wake unakuwa mkubwa kuliko wa wachezaji wake takribani 20. Yaani wachezaji wanaofikia mshahara wa Sh milioni 2, hawawezi kufika 15).


Baada ya kupata saa ambayo ni Sh 2,520,000 ukiipigia mara 24 ili kupata siku, inakuwa ni Sh 60,480,000. Hapa pia unaweza kuanza kushangaa mapema kwamba mshahara wake wa siku moja, unazidi mishahara ya wachezaji wa takribani timu 12 za ligi kuu kwa mwezi?


Kwa fecha hizo, utakapoamua kupata malipo ya mwezi, basi kocha Lechantre anachukua kitita cha Sh bilioni 1.8 ambazo pia zinazidi gharama ya kikosi cha Simba kizima ambacho kimesajiliwa kwa Sh bilioni 1.3.


Kama Simba itakaa naye kwa mwaka mzima, maana yake ni Sh bilioni 21 na chenji kiasi. Kama unakumbuka, mwekezaji mkubwa Simba ni Mohammed Dewji maarufu kama Mo Dewji ambaye anawekeza kwa Sh bilioni 20 na matarajio apate hisa za asilimia 49 au 50. Sasa jiulize, uwekezaji wake wote unaweza kuishia kwa kocha pekee tena ndani ya mwaka mmoja, wa nini sasa?


Kama kweli ni hivyo, hii itakuwa Simba ya ajabu zaidi kutokea katika maisha yote. Kama kocha huyo atapata mshahara huo Tanzania, basi Simba bora wangejenga uwanja wao na wakaamua kubaki na Masoud Djuma.


Thamani ya Uwanja wa Taifa ambao ni mzuri kuliko yote Afrika Mashariki na Kati ni Sh bilioni 53 zilizochangwa na Serikali ya Tanzania na China.


Sasa kama Sh bilioni 21 zingejengewa uwanja, Simba ingekuwa na uwanja ghali na mzuri zaidi kuliko viwanja vyote vinavyomilikiwa na klabu kwa Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.


Kuna mtu mmoja alijaribu kunifafanulia na kusema kwamba walioripoti walikuwa wanamaanisha kuwa kocha huyo analipwa kwa kila dakika katika 90 tu za mchezo.


Hii nayo ikanishangaza pia, kwamba kwani Simba imemuajiri kocha huyo kwa ajili ya mechi tu, yaani zile dakika 90 tu!


Kocha ni mwajiriwa wa Simba na si deiwaka. Anapokuwa katika benchi, kumbuka atakuwa akishiriki katika mazoezi, mikutano na viongozi wa klabu, mikutano na benchi la ufundi. Kumbuka pia hukutana na wachezaji wote au mmoja mmoja.


Sasa unawezaje kumpigia hesabu za mechi kwa mechi katika dakika 90. Wakati mwingine nilifikiri nisijadili ili kujiaminisha huenda hao walioripoti walikuwa wanatania tu!


Kama ni kweli basi haya yatakuwa maajabu ya karne kutoka katika mpira wa Afrika na huenda hata yeye Lechantre atajionea maajabu makubwa kuwa na mshahara takribani nusu ya ule anaolipwa Paul Pogba kule Manchester United.



Sikutaka kuingia ndani sana, nilitaka kuonyesha kiasi gani nimeshangazwa na hilo. Lakini nitasubiri taarifa sahihi ya Klabu ya Simba kama watakubali kutangaza lakini nitafuatilia kujua usahihi, ikiwa ni hivi kweli, nitarudi tuchambue na kushangaa zaidi.

EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati. BOFYA HAPA KUJIUNGA NA INNOVATION FURSA CHALLENGE http://www.edusportstz.com ni fahari ya wasomaji
UNGANA NASI KUPITIA LIKI HIZI ILI KUTUMIWA HABARI POPOTE ULIPO


EDUSPORTSTZ NI FAHARI YA WASOMAJI

WEKA EMAIL YAKO:


Delivered by EDUSPOTSTZ
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno
EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz