MAPOKEZI YA LISSU UBELGIJI NI KUFURUU - EDUSPORTSTZ

Latest

MAPOKEZI YA LISSU UBELGIJI NI KUFURUU


Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antipas Lissu amewasili katika uwanja wa ndege jijini Brussels, nchini Ubelgiji ambapo amepelekwa kwa ajili ya awamu ya tatu ya matibabu yake yatakayohusisha mazoezi ya viungo.

Tundu Lissu amewasili jijini hapo akitokea katika Hospitali ya Nairobi, nchini Kenya alikokuwa anapatiwa matibabu kwa muda wa takribani miezi minne sasa, kutokana na kushambuliwa kwa risasi.

Mbunge Tundu Lissu, ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa kambi ya Upinzani Bungeni, alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana, alipokuwa akitokea Bungeni, majira ya saa 7 mchana, karibu na nyumbani kwake Area D, Mjini Dodoma.

Kwa Mujibu wa taarifa ya madaktari waliokuwa wanamtibu, walieleza kuwa jumla ya risasi 16 zilimpata Tundu Lissu mwilini mwake, na wamefanikiwa kuzitoa, isipokuwa moja ambayo iko nyuma ya uti wa mgongo wake.

Tundu Lissu alieleza kuwa wataalamu na madaktari wake walishauri kuwa risasi hiyo ni hatari zaidi kama ikitolewa kuliko ikibaki ndani ya mwili wake, kutokana na eneo ilipokwama.

==>Picha za Mbunge Tundu lissu alipowasili jijini Brussels kwa ajili ya matibabu zaidi.





TOA MAONI YAKO JUU YA HABARI HII
EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati. BOFYA HAPA KUJIUNGA NA INNOVATION FURSA CHALLENGE http://www.edusportstz.com ni fahari ya wasomaji
UNGANA NASI KUPITIA LIKI HIZI ILI KUTUMIWA HABARI POPOTE ULIPO

EDUSPORTSTZ NI FAHARI YA WASOMAJI

WEKA EMAIL YAKO:


Delivered by EDUSPOTSTZ
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno
EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz