LISSU KUPELEKWA THE HEGUE KWA MASHITAKA HAYA - EDUSPORTSTZ

Latest

LISSU KUPELEKWA THE HEGUE KWA MASHITAKA HAYA




CYPRIAN Mujura ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa CZ Information & Media Consulotant LTD, leo kautaarifu umma kuwa kupitia wanasheria na mawakili maarufu hapa nchini wanakusudia kumfungulia mashtaka katika mahakama ya ndani na ya Kimataifa (The Heque) Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissukwa kauli zake dhidi ya serikali.

Majura amesema hayo leo Jumatatu, Jan. 15, 2017 akizungumza na wanahabari na kusema kuwa, katika Kipindi cha Focus on Africa kinachorushwa na BBC wakati akihojiwa na mwandishi Victor Kenani wiki mbili zilizopita, Tundu Lissu anadaiwa kusema Tanzania kwa sasa ni nchi hatarishi kwa siasa pamoja na pamoja na wote wanaohoji utendaji wa Serikali.


“Alisema watu wanauawa hovyo wanatupwa baharini kwenye viroba, tunataka atupe uthibitisho wa madai yake hayo ndani ya siku mbili zijazo kuanzia leo,” alisema Majura.


Majura amedai kauli hizo ni hatarishi kwa usalama wa nchi, na kwamba inaondoa amani ya nchi iliyoachwa na waasisi wa Taifa hili huku akieleza kuwa mawakili wamejipanga kumfungulia Lissu mahakama za hapa ndani ya Tanzania na wengine wanajiandaa kwenda Mahakama ya Kimataifa (The Heque).

Lissu yupo nchini Ubelgiji tangu wiki iliyopita, Jan. 6 ambako amelekwa ili kuendelea kupatiwa matibabu zaidi baada ya kujeruhiwa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana nyumbani kwake Area D Mjini Dodoma mnamo Septemba 7, mwaka jana.

EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati. BOFYA HAPA KUJIUNGA NA INNOVATION FURSA CHALLENGE http://www.edusportstz.com ni fahari ya wasomaji
UNGANA NASI KUPITIA LIKI HIZI ILI KUTUMIWA HABARI POPOTE ULIPO

EDUSPORTSTZ NI FAHARI YA WASOMAJI

WEKA EMAIL YAKO:


Delivered by EDUSPOTSTZ
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno
EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz