CZECH TOMAS ALITUPIA MIKONO SOKA LA KULIPWA - EDUSPORTSTZ

Latest

CZECH TOMAS ALITUPIA MIKONO SOKA LA KULIPWA




Mchezaji wa zamani wa Arsenal na taifa la Czech Tomas Rosicky amestaafu soka ya kulipwa.

Rosicky alijishindia mataji mawili ya kombe la FA na kuichezea Gunners kwa kipindi cha muda wa miaka 10 kutoka Borussia Dortmund 2006.

Raia huyo ambaye alianza soka yake ya kulipwa katika klabu ya Sparta Prague anasema kuwa majeraha yamemlazimu kustaafu.
”Siweze tena kuandaa mwili wangu kwa kiwango cha soka ya kulipwa”, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 aliambia mtandao wa klabu ya Sparta.

”Mwili wangu ulikuwa ukiniambia kwa muda mrefu kwamba umechoka”, aliongezea Rosicky.
Facebook Comments
EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati http://www.edusportstz.com ni fahari ya wasomaji
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz