Baada ya ukame wa ushindi katika michezo mitano hatimaye Singida United imerejesha furaha kwa mashabiki wake baada ya kuichapa Lipuli bao 1-0.
Katika mchezo huo uliofanyika leo, Ijumaa kwenye Uwanja wa Namfua Singida, bao pekee la wenyeji
Singida United lilifungwa na Danny Usengimana dakika ya 82.
Kuingia kwa bao hilo kuliamsha kelele kutoka kwa mashabiki wengi waliofurika uwanjani kuipa
sapoti Singida United huku kocha wa kikosi hicho Hans Pluijm akionekana mwenye furaha zaidi.
Nahodha wa Singida United, Mudathir Yahaya alisema wanashukuru kupata ushindi huo na
wanaamini wamewapa furaha mashabiki wao.
"Tunashukuru kupata ushindi kwenye uwanja wa nyumbani.tulipata wakati mgumu kipindi cha
kwanza kwa sababu tulifata mpira wa taratibu waliokuwa wakicheza wapinzani wetu lakini
tulivyoingia vyumbani kocha alituambia tunatakiwa kubadilika na kuwapiga presha wa soka la
haraka ili kuweza kupata bao, "alisema Mudathir.
Naye mshambuliaji wa Lipuli, Seif Karihe alisema hawakuwa na mchezo mzuri kwani walshindwa
kutengeneza nafasi nyingi katika mchezo huo tofauti na wanavyofanya katika michezo mingine
iliyopita.
Singida united iliifululiza kupata sare katika michezo
mitano iliyopita na mara ya mwisho kupata
ushindi ilikuwa Septemba 24 ilipoichapa Kagera Sugar bao
1-0.
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno
No comments:
Post a Comment