LIST YA WACHEZJI KUMI(10) WALIOENDA EPL KWA MBWEMBWE WAKAAMBULIA PATUPU - EDUSPORTSTZ

Latest

LIST YA WACHEZJI KUMI(10) WALIOENDA EPL KWA MBWEMBWE WAKAAMBULIA PATUPU





10.George Weah. Wakati anatoka Ac Milan kuja Chelsea mwaka 2000 kila mtu aliamini wapinzani wa Chelsea wanakwenda kuumia kwani Weah alishakuwa mchezaji bora wa dunia, lakini ndani ya miezi mitano alifunga mabao mawili tu Epl akapelekwa Man City.

9.Mario Jadel. Wanasema huyu alikuwa akionekana kama Pele mpya kwani akiwa Gremio alifunga mabao 67 katika mechi 73 lakimi alipofika Bolton alifunga mara 3 tu katika mechi 12.

8.Radamel Falcao. Mashabiki wa United walitamba sana wakati akienda United kwa ada ya £46m lakini alichokifanya walishangaa alofunga mabao 4 katika mechi 29 kabla kwenda Chelsea alikofunga 1 katika mechi 12 lakini alipokuwa Porto alifunga mabao 72 katika michezo 87, Monaco 13 katika michezo 20.

7.Paulo Futre. Hii ilikuwa 1996 huyu alianza cheza timu ya taifa Ureno akiwa na miaka 17 tu, mwaka 1987 hadi 1989 alishinda kombe la Ureno mara mbili lakini aliposajiliwa West Ham alicheza michezo 9 tu na kiwango alichoonesha kilitosha kukatisha mkataba wake.

6.Branco. Mwaka 1994 alikuwa na kikosi cha Brazil kilichoshinda kombe la dunia na mwaka 1996 klabu ya Middlesbrough walimsaini, alipokuwa Middlesbrough alipwaya sana kiasi kwamba baada ya michezo 11 tu mwaka 1997 waliamua kuachana naye.

5.Juan Sebastian Veron. Kama ilivyo kwa Falcao, Manchester United wanawapa Chelsea mzigo mwingine, wakati Veron anakuja United alianza vyema sana lakini baada ya mda alianza kuwa flop na inatajwa ugomvi wake na SAF ndio ulichangia akauzwa Chelsea 2003 ambapo ndiko aliboronga zaidi.

4.Andriy Shevchenko. Hakuna kitu mashabiki wa United, Arsenal na Liverpool waliogopa kama usajili wa Chenko kwenda Chelsea, wataachaje ogopa wakati mshambuliaji huyu alifunga mabao 173 alikotoka? Lakini huwezi amini akiwa na Chelsea alizima kwani michezo 76 alifunga mabao 22.

3.Davor Suker. Kombe la dunia 1998 alichukua kiatu cha dhahabu na alishinda La Liga 1997 na Champions League 1998, ilipofika mwaka 1999 Madrid walimchukua Anelka na wakawapa Arsenal Davor Suker lakini akafunga mabao 11 katika mechi 40 kabla ya Arsenal hawahampeleka West Ham mwaka 2000 alikofunga mabao 3 tu.

2.Angel Di Maria. Usajili mwingine uliojaa mbwembwe sana ni huu, wakati anakuja Manchester United mwaka 2014 kila mtu aliamini moto utawaka, lakini mwaka uliofuta Van Gaal hakuona tabu kumuacha aondoke kwani michezo yake 31 alifunga jumla ya mabao 4 tu.

1.Fernando Morientes. Liverpool walimnunua mwaka 2005 akitokea Madrid alikoshinda Champions League mara 3, mashabiki wa Liverpool walitegemea makubwa kutoka kwake lakini katika michezo 61 aliyoichezea Liverpool alifunga mabao 12 tu.
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz