JOSE MONRINHO AHISIWA KUKACHA EPL - EDUSPORTSTZ

Latest

JOSE MONRINHO AHISIWA KUKACHA EPL




Ripoti kutoka nchini Uingereza hii leo zinasema klabu ya Manchester United imenza kuwa na hofu juu ya kocha Jose Mourinho kwani anahisiwa kuikimbia ligi ya Epl kutokana na ushindani mkubwa.

Pep Gurdiola anatajwa kama sababu ya kumkimbiza Jose Mourinho kwani inaonekana Mourinho anaamini kwa sasa hawezi kushindana na Pep Gurdiola anayeonekana kuwa tishio kubwa hivi sasa.

Jose Mourinho anahusishwa na kutua katika klabu ya PSG tetesi ambazo zilishawahi kuibuka mara ya kwanza lakini baadae zikazima lakini hivi sasa inasemekana kuna ukweli kuhusina na jambo hilo.

Inadaiwa kwamba kutokana na umaarufu na upinzani wa muda mrefu kati ya Jose Mourinho na Pep Gurdiola inamfanya Mreno huyo kujisikia vibaya pale anapoona Pep ana kikosi kinachoonekana kutozuilika.

Pamoja na kiasi cha £300m ambacho United walitumia katika usajili uliopita lakini Mourinho anadaiwa kuhitaji tena kufanya usajili mwingine suala ambalo mabosi wa United ni ngumu kulitekeleza.

Mourinho ndio kwanza yuko nusu ya mkataba wake ambapo aliahidi msimu huu anaweza kufanya makubwa, japo hadi sasa hawako katika nafasi mbaya lakini tayari ameshawahi kuongelea kutamani kwenda Ufaransa.

Katika moja ya mahojiano yake Mourinho alisema hatamaliza kazi yake ya ukocha katika United na akisema Paris kuna jambo maalum huku akikiri hata mwanae alifurahi alipoekwenda Paris akaona mechi ya PSG.

Hadi sasa Manchester United wako nafasi ya pili Epl wakiwa na alama 23 ikiwa ni nane nyuma ya City walioko kileleni na alama 31 huku timu yao ikiwa imefunga mabao 50 katika mashindano yote tangu kuanza kwa msimu.
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz