KILICHO MZUIA JPM KUTOBOMOA JENGO LA TANESCO AKIWA WAZIRI HIKI HAPA - EDUSPORTSTZ

Latest

KILICHO MZUIA JPM KUTOBOMOA JENGO LA TANESCO AKIWA WAZIRI HIKI HAPA



Rais John Magufuli.

Rais John Magufuli amesema aliyekuwa Waziri Mkuu katika serikali ya awamu ya nne, Mizengo Kayanda Pinda, alimzuia kubomoa jengo la Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) lililopo Ubungo, wakati huo akiwa waziri wa ujenzi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kampasi ya Mloganzila leo, Rais Magufuli alisema mbele ya Pinda, aliyehudhuria hafla hiyo kuwa, alitii agizo hilo kwa vile aliogopa kufukuzwa kazi, lakini sasa akiwa rais, hana wa kumuogopa.

“Nilishatoa maagizo, najua Mizengo Pinda kwenye hili alinipinga wakati ule, lakini najua leo hawezi akanipinga kwa sababu mimi ndiye Rais. Wakati ule nilikuwa waziri wake, ndiyo maana nilinyamaza nilijua ninaweza nikafukuzwa, hutakiwi kumpinga mkubwa.

“Hilo jengo la Tanesco, narudia kama itakuwa ni kubomoa nusu, no problem (hakuna tatizo); kama ni lote hakuna tatizo, pamoja na jengo la wizara ya maji. Najua katibu mkuu wa wizara ya maji yupo hapa ananiangalia, wakaanze kulitoa eneo lililopo kwenye hifadhi ya barabara,” amesema.

Waziri Mkuu Pinda wakati huo, alimzuia Magufuli kuchukua hatua hiyo mwaka 2011 akisema ubomoaji huo utasitishwa hadi hapo serikali itakapotoa kauli nyingi juu ya suala hilo, kitu ambacho hakikuwahi kutokea hadi waziri huyo wa ujenzi aliposhinda na kuwa rais wa awamu ya tano wa Tanzania mwaka 2015.

Pinda alikuwa akizungumzia hatua ya Magufuli aliyekuwa amewaagiza wananchi waliojenga nyumba ndani ya hifadhi ya barabara kuanza kubomoa nyumba hizo na wasitarajie kulipwa fidia.

EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati http://www.edusportstz.com ni fahari ya wasomaji
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz