Jorge Delhon amejiua mwenyewe baada ya jina lake kutajwa kuhusika na rushwa mjini New York
Afisa wa zamani wa soka nchini Argentina amejiua baada ya kuhusishwa katika kashfa ya rushwa iliyotajwa mjini New York.
Jorge Delhon amejirusha kwenye reli na kukanyagwa na treni kwenye mji mkuu wa Argentina Buenos Aires.
Baadhi ya viongozi wa soka nchini Argentina wameelezea kusikitishwa na tukio hilo na kusema limetia doa kwenye soka la nchi yao.
Kesi ya Delhon iliyofunguliwa siku ya Jumatatu inafuatia upelelezi wa muda mrefu uliofanywa na Marekani kwenye shirikisho la soka duniani FIFA. Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno
No comments:
Post a Comment