SAMATTA KAWAACHA WATU MIDOMO WAZI TUZO ZA FIFA - EDUSPORTSTZ

Latest

SAMATTA KAWAACHA WATU MIDOMO WAZI TUZO ZA FIFA





Jana kulitolewa Fifa The Best 2017 pale mjini London Uingereza, katika utoaji wa tuzo hizo
manahodha wa timu za taifa dunia nzima walipewa nafasi kupiga kura kumpata mchezaji bora.

Tanzania nao walikuwa moja ya wapiga kura huku nahodha wa timu yetu ya taifa Mbwana Alli Samatta kituwakilisha kufanya zoezi hilo, na tofauti ya matarajio ya wengi Samatta alifanya kitu tofauti kabisa.

Kwa sasa dunia nzima inawazungumzia Lioneil Messi na Cristiano Ronaldo kama wachezaji wakubwa kuwahi kutokea duniani, lakini kwa Samata hali ilikuwa tofauti na inaonekana hawakubali wote wawili.

Samatta kwenye kura zake tatu hajamuweka Cristiano wala Messi badala yake amempigia kura Ngolo Kante kiungo wa Chelsea, pia akampigia mshambuliaji wa PSG Neymar na kisha akampigia Muafrika mwenzake Pierre Aubemayang.

Hata hivyo kati ya wachezaji wote ambao Samatta amewapigia kura ni Neymar pekee ndio amefanikiwa kuingia kwenye tatu bora ya tuzo za mchezaji bora wa kiume huku tuzo ikienda kwa Cr7.

 like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika Propellerads

For Booking>>>



CALL>>>

Voda: +255757441463

JIUNGE NAMI KUPITIA LINK HIZI










Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz