MASHABIKI KAMA HAWA NI KERO KWA JOSE MOURINHO - EDUSPORTSTZ

Latest

MASHABIKI KAMA HAWA NI KERO KWA JOSE MOURINHO





Kocha wa Manchester United Jose Mourinho amewatupia lawama mashabiki wa klabu ya Manchester United kwa kitendo cha kutokumuunga mkono mshambuliaji wao Romelo Lukaku.

Jose Mourinho anasema ameshangazwa sana na mapokezi ya Lukaku katika mchezo dhidi ya Tottenham na kusisitiza kwamba sio jambo la kiungwana kufanya hicho wanachofanya mashabiki wa United kwa sasa.

Mourinho anasema Romelu Lukaku anawapa Manchester United kila kitu alichonacho na anapambana kwa ajili ya timu hivyo haoni sababu ya mashabiki hao kumfanyia roho mbaya mchezaji huyo.

Mourinho amewataka mashabiki wa United kukumbuka mabao aliyowafungia klabu hiyo na kusema kwamba kwa anavyojitolea Mbelgiji huyo hakuna tofauti akifunga mabao na asipofunga.

Mourinho amesema anahisi mashabiki ambao wanamponda Romelu Lukaku kwa sasa watakuwa sio mashabiki wa Manchester United na labda watakuwa na klabu nyingine, Lukaku ana mechi 3 sasa za Epl hajafunga bao lakini ana mabao 7 katika mechi 10 alizoichezea United tangu ajiunge nao.
 like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika Propellerads

For Booking>>>



CALL>>>

Voda: +255757441463

JIUNGE NAMI KUPITIA LINK HIZI










Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz