TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - EDUSPORTSTZ

Latest

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


74 WACHUKUA FOMU, KUREJESHA TFF

Wanafamilia 74 wa mpira wa miguu, wamechukua na kurejesha fomu za kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Agosti 12, mwaka huu.

Hadi zoezi hilo linafungwa leo Juni 20, 2017 saa 10.00 jioni wagombea wote wamerejesha ambako kwenye nafasi ya urais, jumla ya wagombea 10 walijitokeza kuomba nafasi hiyo wakati kwenye makamu rais wamejitokeza sita.

Wadau 58 wamejitokeza kuwania nafasi za ujumbe wa kamati ya utendaji katika Katika Kanda mbalimbali. Zoezi la kuchukua na kurejesha fomu kwa mujibu wa Kanuni ya 10, limefanyika kwa siku tano kuanzia Juni 16, 2017 hadi Juni 20, mwaka huu.

Siku ya kwanza ilipoanza tu, Jamal Malinzi alikuwa wa kwanza kuchukua fomu na kurejesha huku akifuatiwa na Imani Madega, Wallace Karia, Fredrick Masolwa, Athumani Nyamlani, Fredrick Mwakalebela, John Kijumbe, Shija Richard, Ally Mayay na Emmanuel Kimbe.

Waliojitokeza kuwania Makamu wa Rais na kurejesha fomu wako Mulamu Ng’hambi, Michael Wambura, Geofrey Nyange, Mtemi Ramadhani, Robert Selasela na Stephen Mwakibolwa.

Wajumbe wa Kamati ya Utendaji kwa kufuata Kanda 13 ni kama ifuatavyo:

Kanda Na. 1 Mikoa ya Kagera na Geita;

Soloum Chama
Kaliro Samson
Leopold Mukebezi
Abdallah Mussa

Kanda Na. 2 Mikoa ya Mara na Mwanza;

Vedastus Lufano
Ephraim Majinge
Samwel Daniel
Aaron Nyanda

Kanda Na. 3 Mikoa ya Shinyanga na Simiyu;

Benista Rugora
Mbasha Matutu
Stanslaus Nyongo

Kanda Na. 4 Mikoa ya Arusha na Manyara;

Omari Walii
Sarah Chao
Peter Temu

Kanda Na. 5 Mikoa ya Kigoma na Tabora;

John Kadutu
Issa Bukuku
Abubakar Zebo
Francis Michael

Kanda Na. 6 Mikoa ya Katavi na Rukwa;

Kenneth Pesambili
Baraka Mazengo

Kanda Na. 7 Mikoa ya Mbeya, Songwe na Iringa;

Elias Mwanjala
Cyprian Kuyava
Erick Ambakisye
Abousuphyan Silliah

Kanda Na. 8 Mikoa ya Njombe na Ruvuma;

James Mhagama
Golden Sanga
Vicent Majili
Yono Kevela

Kanda Na. 9 Lindi na Mtwara;

Athuman Kambi
Dunstan Mkundi

Kanda Na. 10 Mikoa ya Dodoma na Singida;

Hussein Mwamba
Mohamed Aden
Mussa Sima
Stewart Masima
Ally Suru
George Benedict

Kanda Na. 11 Mikoa ya Pwani na Morogoro;

Charles Mwakambaya Gabriel Makwawe
Francis Ndulane
Hassan Othman

Kanda ya 12. Mikoa ya Kilimanjaro na Tanga

Khalid Mohamed
Goodluck Moshi
Thabit Kandoro

Kanda Na. 13 Mkoa wa Dar es Salaam

Emmanuel Ashery
Ayoub Nyenzi
Saleh Alawi
Shaffih Dauda
Abdul Sauko
Peter Mhinzi
Ally Kamtande
Said Tully
Mussa Kisoky
Lameck Nyambaya
Ramadhani Nassib
Aziz Khalfan
Jamhuri Kihwelo
Saad Kawemba
Bakari Malima

Kwa siku tatu, kuanzia kesho Juni 21 hadi 23, mwaka huu kwa mujibu wa kanuni ya 11.1 ya Uchaguzi wa TFF, Kamati ya Uchaguzi itaanza mchujo wa awali kwa wote waliojitokeza kuwania nafasi mbalimbali kama inavyojionesha hapo juu.

…………………………………………
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz