March 28 2017 shirikisho la soka duniani FIFA lilitangaza kumfungia michezo minne nahodha wa timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi kwa kudaiwa kumtolea lugha mbaya Muamuzi wa akiba.
Messi ambaye alifungiwa michezo minne na FIFA baada ya hapo, tayari amekosa game moja dhidi ya Bolivia ambayo ilimalizika kwa Argentina kupigwa 2-0.
Leo May 5 2017 baada ya Lionel Messi na Argentina kukata rufaa, FIFA imeamua kumruhusu Lionel Messi aendelee kuitumikia timu yake ya Argentina kama kawaida wakati huu ambao shauri lake la rufaa linaendelea kusikilizwa
No comments:
Post a Comment