Tangu siku yangu ya kwanza nilipowasili, nilihisi mapenzi ya klabu hii kubwa na nguvu ya mashabiki wake wa kipekee.
Pamoja tumepambana, tumesherehekea, na tumekua imara zaidi kupitia kila ushindi na kila changamoto tuliyokutana nayo.
Ninatoa shukrani zangu za dhati kwa Rais Mo Dewji kwa uongozi wake wa kipekee, maono yake ya mbali, na msaada usioyumba.
Kwa wachezaji: endeleeni kupigana, kuamini, na kulitetea beji la Simba kwa heshima na kujituma.
Kwa benchi la ufundi na menejimenti: asanteni kwa imani yenu kwangu na kwa kazi kubwa mnayofanya nyuma ya pazia.
Kwa mashabiki wa Simba: ninyi ndiyo moyo wa klabu hii. Sauti zenu, nyimbo zenu, na mapenzi yenu yasiyokoma yatabaki milele moyoni mwangu. Asanteni kwa kuwapokea familia yangu kama sehemu ya familia ya Wanamsimbazi.
Simba daima itabaki kuwa sehemu ya maisha yangu, na ninaitakia klabu hii mafanikio yasiyo na kikomo, neema, na mataji mengi zaidi yajayo.
Asanteni sana, daima Nguvu Moja.
Usikose kutazama mechi ya YANGA VS PAMBA JIJI na SIMBA VS FOUNTAIN GATE, pia na mechi za LIGI KUU TANZANIA BARA, MECHI ZA ULAYA, MASHINDANO YA CAF LIVE bure kupitia Simu yako download App yetu mapema itakayokuwezesha kuzitazama mechi hizi live bure pia ndani ya App yetu utaweza kutazama chanel za Azam tv na Dstv bure bonyeza HAPA au Bonyeza HApa Au hapa pia kudownload app kumbuka app bado hatujaiweka playstore hivo utaidownload kama Apk ikileta neno harmful usiogope.


Post a Comment